Jumatatu, 4 Juni 2018
TABIA MUHIMU ZA MWANADAMU KUFIKIA MAFANIKIO
Kila niangaliapo na kuzichunguza tabia za watu fulani hunipa jibu kuwa kuna tofauti kubwa za tabia za watu katika maisha ya mafanikio.Tabia hizo huonekana pale ambapo mtu anapopata pesa nyingi na pia anapokosa pesa.Wahenga walisema "Pata pesa ujue tabia yako"Hii inamaanisha kuwa watu wengi wakipata pesa hubadilika tabia,hubadilika staili ya mavazi,hubadilika kuongea kwao,hubadilika kutembea kwao.
Leo katika makala haya nimekuletea tabia kuu tatu ambazo mwanadamu anazo wakati akipata pesa.Tabia hizi zinaakisi mwenendo mzima wa maisha ya wanadamu wote na ndio tabia kuu zilizoidhinishwa na Chuo kikuu cha kimataifa cha Havard.
1:MTUMIAJI
Huyu ni mtu ambaye akipata pesa huwaza kutumia kwa anasa na mambo mengine ambayo hayana maaana katika maisha yake.
Mtu huyu hajui ya kesho wala hajui kuwa kuna kukosa hivyo hudumia pesa yake kwa anasa za kila aina ambazo hazina faida katika maisha yake.
Kama ulishawahi sikia stori za mtu akikuambia kuwa
"Hapo zamani nilikuwa nahudhuria katika baa ya DDC kila siku ya jumamosi na jumapili"
"Nilikuwa nalipwa Shilingi ELfu hamsini,mshahara wangu ulilingana na mshahara wa mkurugenzi"
Chunguza maisha ya mtu huyo aliyekuwa akihudhuria Baa kila siku za mapumziko kuwaangalia Jazz Band na kucheza muziki,Juhudi alizoweka kuangalia Muziki ngeweka kuatika uweklezaji angekuwa na mali nyingi pengine kuliko alizonazo sasa.
2: MTUNZAJI
Huyu ni mtu yule ambaye anaenda kutunza pesa benki kwa muda mrefu pasipo kumzalishaia kwa Lugha ya uswahilini watu hawa wanaitwa "wabahili" Mara nyingi watu hawa husikitika sana pale wanapoona pesa zao zikitumika kwa uzalishaji,hufikiri kuwa pesa ikiwekezwa inaweza kupotea na asiipate nyingine tena.
Mara kwa mara watu hawa hutunza pesa zao kwenye maroba,mabenki au huchimbia chini ya ardhi,huishi maisha ya kawaida kabisa ambayo si rahisi mtu mwingine kumjua kama ana kiasi kikubwa cha pesa.
3: MWEKEZAJI
Mtu mwenye tabia hii ndio mwenye mafanikio makubwa,watu hawa ndio wanaoongoza dunia,ndio wanaomiliki mali nyingi na kumiliki viwanda vikubwa ambavyo ndio hutoa ajira nyingi.Watu wenye tabia hii hutamani kuwekeza kila pesa inayopita mikononi mwao,wako tayari kuwekeza pengine wasibakiwe hata na shilingi mikononi mwao.
Hizi ndio tabia kuu tatu ambazo mwanadamu amezaliwa nazo,tabia hizi zinaweza kubadilika kulingana na mazingira uliyonayo ingawa haziwezi kufutika kabisa.
Mara nyingi tabia hizi hubadilika na kukomaa pale unapoambatana na mwenye tabia kama yako,hushindwa kukomaa na hubadilika kutoka kwenye tabia nyingine pale unapoambatana na mtu mwenye tabia isiyofanana na tabia yako.
Asante sana wako Bundala Abely Izengo
Jumamosi, 2 Juni 2018
KUWA MWANDISHI WA FILAMU YA MAISHA YAKO
Uandishi ni moja ya kazi ambayo inahusu kukusanya habari na kuzichambua kwa kina kwa dhumuni la kutaarifu umma,lakini kwenye makala haya namwelezea mwandishi wa filamu ambaye anaandika filamu ya muongozo wa maisha yake ambaye ni wewe,ndio wewe ni mwandishi mzuri au mbaya wa filamu ya maisha yako.
Mwandishi mjuzi wa filamu huandaa mwongozo mzuri kuanzia mwanzoni na mwisho wa filamu yake,hupangilia wahusika katika vipengele mbalimbali vya filamu husika.Mwandishi huandaa muongozo wa filamu ambayo huanza kumpa picha halisi kabla ya kuanza kuicheza filamu hiyo.
Katika kuandika filamu ya maisha yako,wewe kama mwandishi ni lazima uwe na washiriki wakubwa watatu ambao ndio hukamilisha sinema ya maisha yako.
1)MTAZAMAJI
Huyu ni mtu ambaye anatizama jinsi ambavyo sinema ya maisha ya wengine inavyoendelea, huyu hukubali na kupongeza baadhi ya vipande vya maisha ya wengine na kuviponda au kuvikosoa baadhi ya vipande hivyo.Aina hii ya watu ni watu wa kwenye vijiwe vya kahawa,bao au kamali huwa ni watu wa kutoa maoni juu ya maisha ya watu,hawa ni watu walio duni katika maisha yao,watu wasio kuwa na ndoto katika maisha yao.
Ni watu ambao hawajuo kupambanua nyakati hukosoa juhudi za watu wengine.
Mfano "Fulani kanunua gari amehongwa na mtu fulani:" autasikia
"Huyu ana nyumba nzuri ameibia kampuni fulani"
Epuka vikao vya watazamaji hawa ambao wanatazama filamu za wengine zikiendelea mbele.
2) MWIGIZAJI
Mwigizaji ni mhusika mkuu katika filamu ya maisha na anajua kuwa yeye ni mhusika mkuu na anaweza kuongoza sehemu kubwa ya filamu ya maisha yake.Anaweza kujenga au kubomoa filamu ya maisha yake kwa jinsi ambayo anaweza kuuvaa uhusika katika maisha na jinsi ambavyo anaweza kuusaliti uhusika wake.
Mwigizaji huwa na furaha katika maisha yake kwa sababu anajua kuwa yeye ni mshindi na ufurahia maisha ya aina yoyote ile pia hufahamu kabisa kuwa filamu ya maisha yake inaweza kuisha kwa namnna yeyote ile na yuko tayari kwa lolote.
3) MWANDISHIA MWIGIZA
Huyu ni mtu yule ambaye haangalii tu na haigizi tu lakini ni yule ambaye anatengeneza sinema kutoka kichwani kwake.anajua nini ataongea,atafanya kipi na mwisho wa sinema utakuaje .
Mtu huyu ana uwezo mkubwa wa kuendesha maisha yake na anajua kabisa maisha yake yatakuwa mazuri au mabaya.
Mtu huyu huwa makini sana katika kujenga maisha yake.Watu wengi waliofanikiwa wapo katika kundi hili,ni waandishi,waigizaji na waongozaji katika sinema za maisha yao.
Swali la kujiuliza
Je wewe ni mtizamaji?
Je wewe ni mwigizaji ambae unaigza kwenye filamu usiyoijua mwisho wake?
Au wewe ni mwandishi na mwongozaji wa filamu ya maisha yako?
Maisha yako, yako mikononi mwako ni wajibu wako sasa kutengeneza au kubomoa,kuwa mwandishi,mwigizaji au mtazamaji.
Asante sana kwa muda wako kwa kusoma makala haya.
Ndimi Bundala Izengo 0656669989.
Jumatano, 23 Mei 2018
HATUA KUU TATU ZA KUFIKIA NDOTO YAKO
Unaweza kushangaa kwa nini hupati kile unachokitafuta!Je unajua sababu ya kushindwa kutimiza ndoto zako ni wewe mwenyewe?
Utakubaliana na mimi kuwa sababu ya kushindwa kutimiza ndoto zako ni kwa sababu haujui nini unakitafuta na unakihitaji.
Watu wengi wamekuwa na hamu ya kupata mafanikio makubwa lakini wameshindwa kutofautisha hamu/shauku zao ambazo zimegawanyika katika viwango vitatu vya uhitaji.
Viwango hivi vitatu ambavyo vitakusaidia wewe kujua upo katika kiwango gani,pengine kupiga hatua kutoka katika kiwango ulichonacho kwenda kwenye kiwango kinachofuata
1. KIWANGO CHA "NINGEPENDA"
"Ningependa" neno hili huonyesha upenzi wa kitu fulani ambacho mtu anapenda kukipata au kuwa.Mfano Ningependa kuwa raisi,Ningependa kuwa tajiri.,,
Ningependa kuwa mfanya biashara mkubwa.Watu wengi wako katika kundi hili la kutaka kuwa mtu fulani lakini katika kundi hili hutumika nadharia tu, hakuna kitendo chochote kitakachotokea katika kiwango hiki cha kupenda.
2. KIWANGO CHA "KUTAKA"
Katika hatua hii watu husema nataka kuwa mtu fulanii ninataka kuwa mwandish mzuri,ninataka kuwa mwalimu mzuri.
Hatua hii inakusanya maandalizi madogomadogo pia ni hatua muhimu ya mwanzo inayokusanya vitendea kazi kwa ajili ya kuvitumia katika kusudio lako.
Kiwango hiki sio kiwango ambacho kinakuweka katika kilele cha mafanikio lakini ni kiwango cha pili cha muhimu cha maandalizi ya kukuweka kwenye kilele.
3. HATUA YA KUJITOA (KUFANYA KAZI)
Katika hatua hii ndipo watu huanza kufanya kile ambacho ndoto yao inataka iwe,bidii ndio funguo muhimu ambayo mtu anapaswa awe nayo katika kufanikisha jambo lake na kupiga hatua zaidi.Dhamira ndio kiini cha mambo yote kwa kunafanya kile ambacho umekidhamiria,kile ambacho kimekuwa ni ndoto yako ya kila siku.
Dhamiria kikamilifu katika ndoto zako,fanya kazi kwa bidii bila kuchoka,weka mipango na mikakati ya kuendeleza na kupanga ndoto zako hakika utakuwa umepiga hatua kubwa kimaendeleo na utaweza kufikia malengo yako na kupata kile unachkitafuta.
Ukawe na siku njema msomaji wangu wa mtandao wa www.patamamboadress.com
Ni mimi Mwandishi wa makala hii Bundala Izengo.a
Jumapili, 21 Januari 2018
HIVYO ULIVYO NI ZAO LA MAWAZO NA TABIA YAKO
Ni tumaini langu kuwa haujambo rafiki yangu mpendwa na msomaji wa blog hii ya patamambo,leo katika makala haya ninakwenda kuangazia nguvu ya MAWAZO inavyoweza kubadilisha maisha yako hata ulimwengu.
Wazo ni nguvu ambayo imeleta mabadiliko makubwa katika dunia hii,uumbaji wa dunia na mali zote zilizopo ulianza na wazo.Mungu alimuumba Adamu baada ya kumuumba Adamu Mungu ALIWAZA Haipendezi mtu huyu kuishi peke yake ndipo alipompatia msaidizi wake ambaye kwa jina aliitwa Hawa.
Huu ni moja wa mfano ambao nimekupatia ndugu ili uelewe juu ya Nguvu ya Wazo ambavyo imekuwa tangu dunia kuumbwa.Wagunduzi wa sayansi na tekinolojia wote walianza na wazo kisha wazo hilo wakaliweka katika vitendo ndio maana leo tuna simu za mkononi,ndege,mitandao ya kijamii nk.
Je una wazo gani hapo ulipo,wazo lako lina nguvu,Wazo lako lina uwezo wa kukufikisha katika uhuru kifedha,Je wazo lako unaweza kuliweka katika uhalisia na kulifanyia kazi ili likuletee faida na kukupatia kipato?Haya ni maswali unayopaswa kujiuliza kabla ya kuliweka wazo lako katika vitendo.
Maisha yako yanaaksi mawazo yako uliyowaza mwaka uliopita,miezi iliyopita,juzi,jana na leo,maisha uliyonaho sasa umeyatengeneza kwa mawazo yako ya siku za nyuma kwa kujua au kutokujua,nguvu ya wazo lako ndio maisha ambayo unayoyaishi sasa na utaendelea kuyaishi kesho na kesho kutwa.
Sikiliza Rafiki nikuambie Kushindwa sio kitendo cha siku moja,huwezi kushindwa kwa usiku mmoja, kushindwa ni kosa ambalo unalifanya katika mawazo yako ni tabia ya kurudia rudia kosa kila siku hivyo matokeo yake sasa kosa hilo linakuletea matokeo hasi juu ya wazo lako.
Hivyo ulivyo ni zao la mawazo na tabia au matendo yako ambayo unayarudia rudia kuyafanya kila siku.Wewe ni maskini kwa sababu hauna tabia ya kuweka akiba kila mara,ni maskini kwa sababu mawazo yako hayaendani na vitendo vyako vya kila siku.
Asante sana kwa kusoma makala haya ni mimi Bundala A. Izengo 0656669989
Jumamosi, 20 Januari 2018
FANYA HAYA ILI UWEZE KUFIKIA MALENGO YAKO MWAKA 2018
Kwaheri mwaka 2017 karibumwaka mpya wa 2018 hizi ni baadhi ya sauti za watu wengi ambao Mungu amewajaalia kuona mwaka Mpya.
Nianze kwa kukuambia kuwa Hongera sana rafiki kwa kuona mwaka 2018.
Kila mwanzo wa mwaka watu hupanga mipango mingi ili kuweza kusukuma maisha ya kila siku na kutimiza ndoto mbalimbalimbali.Ni vyema ndugu ukawa na mipango ambayo utaenda kuifanyia kazi mwaka huu 2018 na hakikisha kuwa mipango hiyo inafanikiwa kabla ya kumaliza mwaka 2018.
Rafiki unapoanza mwaka mpya kitu pekee kinachobadilika ni namba yaani 2017 - 2018 mambo mengine yote hubaki kama yalivyo,thamani ya pesa hubaki vilevile,masaa huhesabika vilevile,Dunia hulizunguka jua katika staili ileile,pumzi na hewa tunayovuta huwa ni ileile n.k.
Katika mwaka huu 2018 kitu pekee unachopaswa kubadili ni staili ya maisha uliyonayo unahitaji mabadiliko ya kifikra katika kufikia mafanikio yako, unahitaji mabadiliko ya kiroho ili kufikia malengo yako, unahitaji mabadiliko ya kimwili ili kuweza kufikia malengo yako,pia unahitaji kubadili mbinu za kuongeza thamani na faida katika biashara yako au kazi yako ili kweza kufikia malengo yako.
Unapoanza mwaka 2018 unakuwa na uhakika wa asilimia mia (100%) wa kufikia malengo yako,kadri siku zinavyokwenda ndivyo asilimia inavyozidi kupungua.
Mpaka kufikia tarehe 30/12/2018 wapo watakao kuwa wamepunguza asilimia zao za kufikia malengo na kufikia 80,70,10,20,95 hata wengine 98%.
Ningependa kila rafiki yangu katika mtandao huu anafikia malengo yake mwaka huu 2018 bila kujali ukubwa wa malengo hayo.
Fanya haya
1.Chukua Daftari andika malengo yako kumi unayofikiria kuyatimiza mwaka huu.
2. Chambua malengo yako Matano
3.Chambua tena malengo mengine matatu muhimu.
4. Andika lengo lako muhimu moja ambalo utaenda kulifanyia kazi kila kukicha.
Jikumbushe malengo yako muhimu matatu kila siku na ufanyie kazi lengo lako moja kila siku bila kusahau malengo yako mawili muhimu ambayo nayo utayafanyia kazimwaka huu 2018.
Fuatilia blog hii Patamambo ili tuweze kuhamasishana kila siku.
"USIKU HUU WANAITAKA ROHO YANGU"
Aliingia mkuu wa wachawi ambaye alikuwa akitokea Gamboshi iliyoko mkoani shinyanga wilayani Bariadi, kila mchawi alisimama na kuanza kupiga makofi kwa staili ya aina yake,walikunja mikono yao na kufanya kama kuku anayegonga mabawa akitaka kuwika.
Mkuu wa wachawi aliingia akiwa na ungo alitembea kwa kila aina ya madaha huku akifuatiwa na walinzi wake, alitokea mchawi mmoja ambaye alikuwa amebeba mtu ambaye Nipe alimfahamu.Alikuwa ni jirani yake ambaye ni mwenyekiti wa kijiji hicho,mama huyo alikuwa ni mnene na alikuwa na makalio makubwa.
Mkuu wa wachawi alikaa katika makalio ya mama yule ambaye aliwekwa chini na kuanza kikao.
“kwanza kabisa poleni kwa kazi pevu ya kulijenga taifa hili la kichawi ambalo linaongeza mamilioni ya wajumbe, si viongozi wa kisiasa ,watoto ,wakubwa hata maadui zetu wachungaji wametupa biblia na kujiunga na taifa hili.” Alizungumza kwa kujiamini.
Jicho la nipe lilikuwa likimtizama mama yake ambaye alikuwa akiitikia kwa shangwe na kila aina ya furaha .
Sina alikuwa akipika na mabinti wenzake wawili ambao walikuwa wamehudhulia kikao hicho.
Siku hiyo ilikuwa siku ya kufunuliwa kwa Nipe kwani dada zake wote walifariki katika mazingira ya kutatanisha .Baada kuzungumza kwa muda mrefu mkuu wa wachawi alisimama na kuzungumza kwa sauti ya hamaki.
“Nimepata taarifa kuwa kuna mshiriki mwenzetu ambaye alikuwa akipiga chenga ya kutoa kafara yetu ambayo tumejiwekea tangu enzi za mababu zetu, nimekuja kusikiliza malalamiko hayo ambayo leo tutayapatia ufumbuzi.” Mama yake Nipe alivuta pumzi kwa uoga.
“Mkuu hilo lilikuwa likitusumbua katika kambi yetu hii takatifu,mama Nipe amekataa kutoa kafara amekuwa akikataa kwa sababu amebakiwa na mtoto mmoja tu.”alizungumza mmoja wa wachawi aliyekuwa karibu na mama Nipe.
“Naomba tumpatie nafasi ya mwisho siku ya leo atupatie nyama au damu ya mtu ya kutupatia nguvu na kuimarisha uchawi wetu.unayo nafasi mama Nipe tupe mtu ili leo tupate chakula chetu.” Alizungumza mkuu wa wachawi ambaye alikuwa msuluhishi wa migogoro katika matawi ya serikali ya wachawi hapa nchini.
“Mkuu leo sina la kuzungumza zaidi ya kutoa karafa hiyo,kwa heshima na taadhima naomba vijana wako waelekee kwangu katika chumba cha Nipe wakamchukue kwa ajili ya kitoweo katika kikao hiki kitakatifu.”
Wote walishangilia,vijana watatu wenye miraba minne walitumwa kumchukuwa nipe nyumbani kwao kwani mama yake aliamini kuwa atakuwa karudi kutoka kwenye ngoma ya chagulaga.
Vijana hao walisimama na kuchukua usafiri wa ungo,alikimbia kwa spidi kuliko umeme, Nipe alikuwa juu ya mti wa mkwaju akisikiliza kila kilichoendelea,alishtushwa aliposikia mama yake kimtaja kuwa afuatwe ili auwawe.
“kweli mama anazungumza ili mimi niuwawe!”alizungumza kwa mshangao mkubwa huku akitetemeka miguu na mikono hali ambayo matawi ya mkwaju yalianza kutikisika ,Sina aliona hali hiyo na kujisemea kwa sauti kubwa
“Usiogope,kuwa na ujasiri”Mabinti wenzake waliokuwa wakisaidiana naye walimuuliza alikuwa ukizungumza na nani, lakini sina alisema alikuwa akikumbuka jinsi walivyokuwa wakiambiwa vijana wa kisukuma walivyokuwa wakicheza ngoma ya chagulaga.
Vijana waliotumwa walirudi mbio huku wakihema juu juu wakiwa mikono mitupu ,mama Nipe aliuliza kwa hamaki.
“ Yupo wapi mbona mnarudi mikono mitupu?”
“Hayupo tumemkosa kwani tumetazama kila kona ya nyumba tumemuona baba yake akiwa amelala lakini yeye hayupo” vijana walikuwa wametumwa kumfuata walijibu huku wakihema.
Mama nipe alichanganyikiwa alivuta pumzi kwa nguvu kabla hajaongea,mkuu wa wachawi aliuliza swali.
“Mama Nipe unataka kukichezea kikao tukufu cha wachawi ,umemficha mwanao eti” ilikuwa ni sauti ya kutisha ambayo ilionesha kuwa mkuu wa wachawi alikuwa kagadhabiika.Sauti hii iligonga katika ngoma za masikio ya mama Nipe na kumfanya apatwe na mshtuko.
“Nendeni mkamwangalie kwa rafiki yake Ngosha siku ingine huenda kulala huko .”Ilikuwa ni sauti ya mama Nipe ambaye aliamrisha vijana wake waende wakamwangalie Nipe kwa rafiki yake kipenzi ambaye hupenda kutembea naye mara kwa mara .
Vijana walichukua tena usafiri wao wa ungo na kupanda kila mmoja alihakikisha kuwa alikuwa yuko sawa sawia ndani ya ungo ule na kufyatuka.
Nipe alikuwa ndani ya mawazo mazito, mwili ulipigwa na ganzi alijikuta mkojo ukimtoka bila kujijua na kumdondokea bibi kizee aliyekuwa amekaa chini ya mti wa mkwaju.
“Haya maji yanatoka wapi”Aliuliza bibi aliyedondokewa na mkojo,sina hakuchewa kujibu.
“Bibi umekaa karibu na shina,wadudu na ndege hupenda kulala karibu ya shina atakuwa ni mdudu amekojoa .”Sina alizungumza na kumundolea kiti ambacho alikuwa amekalia na kukisogeza pembeni kidogo. Nini kitaendelea fuatilia blog hii
Jumatano, 25 Oktoba 2017
MTUHUMIWA NAMBA MOJA WA KIFO CHA UCHUMI WAKO NI WEWE
Nukuu "Maisha ni magumu na hayajawahi kuwa rahisi" Dr. Makrita
Nimeanza nakuandika nukuu ambayo itaniongoza katika makala haya ambayo nimekuletea siku ya leo.Nukuu hii ni ya Mwalimu wangu wa masuala ya ujasiliamali na uwekezaji Dr. Amani Makrita.
Mwanadamu ameumbwa na lugha ya lawama hasa kipindi anaposhindwa kutekeleza malengo yake,tumesahau ya kuwa matatizo ya kijamii na kiuchumi yapo kila siku, katika mazingira ya sasa utasikia neno hili
"Usawa huu wa Magufuli tutanyooka" Hizi ni sauti za watanzania wengi waliokosa tumaini la kesho na kujaribu kutoa lawama kwa Raisi aliye madarakani,ukitizama kwa mapana neno hilo linaashiria kuwa watu walitegemea kupewa pesa mikononi ama kupanga foleni kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa kwa ajili ya kupewa pesa,hata kama ingekuwa hivyo bado minong'ono juu ya hali ngumu ya maishi isingeisha.
Nadharia hii iko sahihi kwa asilimia 10 pia haiko sahihi kwa asilimia 90 ,serikali inatoa asilimia 10 tu kama mchango wake katika maendeleo ya kila mwananchi.Asilimia hizo kumi hutolewa kwa kupunguza bei za pembejeo na madawa,vitendea kazi,usalama wa raia na mali zake, kusimamia soko la ndani ili kusiwepo na mfumko wa bei n.k
Hizi asilimia 90 unapaswa kuzitafuta wewe,Mafanikio ya malengo yako, yapo mikononi mwako mwenyewe.Hebu fikiria Ndugu yangu, matajiri wa dunia wana mali kedekede lakini mpaka kesho wanaendelea kutafuta pesa bila kuchoka.
Yawezekana kabisa tukalalamika kuhusu ugumu wa maisha, lakini wimbo huu tusimhusihe kiongozi,taasisi wala kampuni fulani kuwa ndio sababu ya ugumu wa maisha huu ni wimbo ambao kila mwana mafanikio aukatae na kuukemea kwa nguvu zote, yawezekana sisi wenyewe tukawa sababu ya hali ngumu ya maisha kulingana na sababu ambazo nitaziorodhesha hapa.
UVIVU WA KUFIKIRI NA KUTENDA
Nikiwa natafakari jinsi ya kuianza siku ya siku ile, nilitizama pembezoni mwa ukuta wa nyumba na kuona majani ya tikiti yaliyotanda kuzunguka ua, lililokuwa karibu na chombo nachotumia kutupa taka kabla hazijaondolewa na Manispaa.
Nilitizama kwa makini Tikiti lile niligundua kuwa kwenye shina lake limebeba watoto watatu (matikiti) yenye ukubwa saizi ya ngumi.
Wazo jipya la biashara lilijengeka kichwani kwangu,nilikimbia mara moja mpaka katika duka la Pembejeo za Kilimo na kununua mbegu bora za matikiti.
Nilinunua jembe na viroba ambavyo vilitumika katika kuandaa shamba la nyumbani,nilipanda mbegu za tikiti katika viroba ambavyo nilivipanga pembezoni kuzunguka nyumba, nilifuata maelekezo yote ya mtaalamu wa kilimo kama alivyonielekeza niponunua mbegu hizo,baada ya miezi mitatu nilivuna jumla ya matikiti 200 ambayo niliyauza kwa shilingi 3,000 kila moja na kupata jumla ya shilingi 600,000/= .
Kama mimi niliweza unasubiri nini,anza leo usisubiri kesho.
Huu mchezo wa Taifa wa kulaumu mtu hatupaswi kuendekeza na kuuendeleza kamwe,tambua ya kuwa wewe ndio mtuhumiwa namba moja katika kosa la kudidimiza afya ya uchumi wako.
Nikiwa katikati ya mazungumzo na baadhi ya vijana wa mtaani kwangu,Nilishtushwa na sauti ileile ambayo vijana wa sasa wanapenda kuitumia.Ally Aliniambia neno hili
"Magufuli kabana kweli ndugu yangu nitoe hata buku kumi!"
Hii ni sauti ya kijana mwenye nguvu ambaye hata kabla ya utawala huu sikuwahi kumuona akifanya kazi yoyote isipokuwa kukaa vijiweni kupiga soga na marafiki zake,huku wakisubiria kengele ya chakula nyumbani kwao
Nilimuuliza swali hili Ally.
"Unasema hali ngumu wala viongozi hawana msaada kwenu mbona Kaka yako Jummanne Jana alifungua biashara mbili mpya,Vipi kuhusu duka jipya la mangi alilofungua hivi majuzi?"Hawa ni baadhi ya watu waliofungua miradi mipya hivi karibuni,Je hawa watu wametoa wapi mitaji ? wakati tunaishi nao Tanzania,Raisi wetu mmoja,Mbunge wetu mmoja, Diwani mmoja sera moja ya nchi,ardhi moja na thamani ya shilingi ni moja?" Jibu lilikuwa
"Kaka michongo imekaa vibaya"
Kila mmoja anaweza kutengeneza kiza nene juu ya Maisha yake,lakini kila mmoja anaweza akatengeneza nuru nzuri katika maisha yake kwa kufanya kazi kwa uadilifu,uaminifu na kujituma ili kufikia mafanikio makubwa.
Bundala anakuambia.
" Usisubiri mafanikio kutoka serikalini, kama unahitaji kufanikiwa anza kuyatafuta mwenyewe,Mafanikio yako, yapo mikononi mwako."
Alhamisi, 28 Septemba 2017
KABLA YA KUANZA BIASHARA/KAZI MPYA FANYA HAYA KWANZA
"Hodi Hodi.....!" Ilikuwa ni sauti ya kijana Mike ambaye sikumtia machoni miaka mitatu iliyopita.
"Karibu sana Kijana Habari za siku nyingi"Ilikua ni sauti ya Bundala Izengo Mwandishi wa Makala haya baada ya kutembelewa na kijana Mike ofsini kwake.
Sura ya Mike ilionekana yenye huzuni,aibu hata asili yake ya kujiamini ilipotea,mikunjo ya ngozi yake na mapere katika paji la uso(chunisi) na ngozi iliyofubaa na kupoteza rangi yake ya asili vilinisababisha kutoa chozi la huruma kwa kijana huyu ambaye alikuwa ni jirani yangu pia rafiki yangu kibiashara.
Si kwa sababu ya maradhi la hasha,hii ni kwa sababu ya maisha magumu aliyonayo baada ya kuacha biashara aliyokuwa anaifanya na iliyokuwa ikimuingizia faida nono baada ya kuambiwa na ndugu zake kuwa kuna biashara ambayo ingemwingizia kipato kedekede,Sio dhambi wala kosa kuacha biashara uliyonayo bali ni kosa kubwa kuacha biashara inayokuingizia kipato bila kufuata taratibu zifuatazo.
1.FANYA UTAFITI WA KUTOSHA
Ni dhahiri kuwa Mike hakuzingatia kipengele hiki muhimu cha uanzishaji wa biashara,hata kama alikifanya basi ni kwa kiwango cha chini kabisa,kipengele hiki kinakusanya mambo mengi ikiwemo kuandaa Mpango wa biashara, ni vyema zaidi ukawashirikisha wataalamu wa mahesabu ya biashara ambao watakusaidia mambo mengi ya kufanya kabla na baada ya kuanza biashara.
2. ZUNGUMZA NA WABOBEVU KATIKA BIASHARA HIYO
Hii ni hatua muhimu kabla ya kuanza kufanya biashara mpya waulize wenyeji wa biashara hiyo mambo mbalimbali yanayohusu biashara unayotaka kuifanya,ikiwezekana omba kazi mahali hapo hata kwa kujitolea ili uweze kujua changamoto za kazi hiyo japokuwa changamoto zingine hauwezi kuzijua mpaka utakapoingia rasmi kwenye biashara hiyo. Wakati hayo yote ukiyafanya usisahau kufanya hili lifuatalo ambalo Mike hakulifanya.
3. USIFUNGE BIASHARA YA MWANZO.
Ghafla Mike alipotea machoni pangu,duka lake akalifunga akawa anakuja kuchukua baadhi ya vitu na kuviuza kwa watu tena kwa bei ya hasara,nilijaribu kumuuliza ni kitu gani kimemkuta aliniambia maneno haya
"Huku mambo yametiki babu njoo tujichanganye kwenye biashara ya kuleta mazao ya viazi Mbatata jijini Dar es salaam" Sikukomea hapo nilijaribu kumshauri neno hili
"Mwachie mdogo wako au ajiri mtu aweze kukuendeshea biashara hii,huko uliko unawezakukwama ukarudi kwenye biashara yako ya awali."Mike alinitiazama kisha akacheka na kuniambia.
"Hapana Bundala,nafanya hivi ili kuongeza mtaji wangu kwani kiasi nilichonacho hakitoshi"Sikuchoka kumuuliza maswali ili niweze kujua faida inayopatikana katika biashara yake mpya,lakini nilipomujliza swali hili ndipo nikaumia zaidi
"Mtaji uliutoa wapi kijana mpaka ukaweza kufanya mambo makubwa kama haya?" Baada ya kunijibu swali langu hili,ndipo nilishangaa na kustaajabu ya Musa na baada ya miaka mitatu niliyaona ya Filauni, Majibu ya swali langu yalikuwa hivi.
4.USIKOPE ILI KUANZISHA BIASHARA MPYA
Watu wengi hufurahia kupata mkopo kwa sababu ni pesa ambayo unaipata bila ya wewe kuteseka wakati wa kuitafuta,sasa jua ya kuwa baada ya kukopa utateseka kuitafuta kwa ajili ya kurudisha mkopo.Kama tayari ulishaanza biashara yako na unataka kubadili biashara ni bora ukaweka akiba yako mpaka itakapojitosheleza.
Majibu ya swali langu yalikuwa ni hivi
"Nilikopa kwenye benki moja,kulingana na dhamana niliyonayo Walikubali kunipatia Milioni 10 hivyo ndio maana nimeanzisha niashara hivyo basi kutokana na ukubwa wa mtaji huo sioni sababua ya kuendelea kufanya biashara hii ya zamani"Alizungumza Mike na kuondoka.Niliwaza juu ya maisha aliyonayo wakati huo,niligundua ya kuwa, kwa mtaji huo Mike atakua ametusua (kufanikiwa).
5. HAKIKISHA UNA AKIBA YA KUTOSHA
Mwalimu wangu wa Ujasiliamali na Uwekezaji Dr. Amani Makrita,aliwahi kunifundisha somo hili ambalo ni muhimu sana endapo utadhamiria kuanza kufanya biashara mpya.Baada ya kupata mafunzo haya nilimkumbuka Kijana Mike Ambaye hakuweza kufuata kanuni hii pengine kwa kujua au kutokujua.Dr. Amani alisema hivi
Unapotaka kubadili biashara,hakikisha umeweka akiba ya kutosha katika akaunti yako,Hakikisha una pesa ya kuweza kuhudumia familia yako kuanzia chakula,malazi,mavazi na kulipia karo za shule kwa muda wa miezi sita ijayo,hakikisha una pesa ya kutosha ya kulipia madeni ya mikopo ya benki/binafsi kwa muda wa miezi sita bila kutegemea pato la biashara yako Mpya,uwe na akiba ya Nusu mtaji wako mpya kwa ajili ya kukabiliana na majanga au hasara.
Hili ndio lilikuwa kosa kubwa alilolifanya Mike ambaye aliingia katika biashara mpya akiwa na mkopo benki,bila ya kuweka akiba ya miezi sita ijayo.Baada ya kufanya biashara kwa muda wa miezi miwili Mike alipata ajari ya gari na kupoteza mali zake zote.
Maisha yaligeuka,alikimbilia kusikojulikana na kuacha mali zake Nyumba,kiwanja alizoweka dhamana zikachukuliwa na benki,Maisha yalikuwa magumu mpaka siku ha kwanza aliporudi mjini, nilijifunza mengi juu ya mkasa huu.
Nina imani unayesoma makala Haya hautaweza kufanya makosa kama ya Mike Jipange katika mambo hayo niliyokuorodheshea pindi unapotaka kufanya biashara Mpya au Kuacha kazi na kufanya kazi/biashara nyingine.
Hadithi hii ni ya kutunga haina ukweli wowote juu ya Maudhui na Majina. Mtindo uliotumika ni mtindo wa Darasa kwa njia ya hadithi.
Asanteni sana ni mimi BUNDALA ABELY IZENGO 0656669989
Jumatano, 6 Septemba 2017
MAMBO YANAYOSABABISHA MATUMIZI MABAYA YA PESA.
Kila kukicha matumizi ya pesa yanazidi kuongezeka hali ambayo inasababisha pesa iwe na majina mengi kama faranga,mshiko,mapene,ndarama,fulusi,senti,mbago,shekeli n.k.Kubadilika kwa majina haya si kwa bahati mbaya bali ni kwa sababu watu wanaipenda pesa na wanaitafuta pesa kila kukicha.
Unaweza kukubali kuwa kuitafuta pesa ni jambo moja na kuitumia pesa ni jambo jingine.Je ni wangapi wanaoitafuta pesa usiku na mchana wakiipata wanakwenda kuweka heshima baa?Je ni wangapi wanaotafuta pesa kwa jasho jekundu lakini matumizi yao yanaishia kwa madada poa?
Leo katika somo letu kwa njia ya hadidhi tutajifunza juu ya MAMBO AMBAYO YANASABABISHA MATUMIZI MABAYA YA PESA.
Katika familia tunazoishi matumizi mabaya ya pesa hurudisha nyuma maendeleo ya familia nilifanikiwa kusikiliza mzozo huu wa wanandoa hawa.
1. MATUMIZI YASIYO YA LAZIMA
"Hodi ndani" Ilikuwa sauti ya Bundala mwandishi wa makala haya alipomtembelea rafiki yake Shafii nyumbani kwake.
"Karibu baba mdogo"Sauti ya Jane (mtoto wa kwanza wa Shafii ilisikika ikinikaribisha) Niliingia ndani na kuketi juu ya kiti.
Ghafla nilisikia minong'ono iliyoashiria kuna shari chumbani kwa Shafii.
"Wewe unatumia vibaya pesa juzi umenunua Dela, Jana gauni leo unataka pesa kwa ajili ya kiatu wakati nguo na viatu unavyo tele!"Hii ilikuwa ni sauti ya rafiki yangu Shafii ambaye alikuwa akimgombeza mkewe kwa kumtuhumu kuwa anatumia vibaya pesa.
Uwepo wangu mahali pale nilihisi wa bahati mbaya,niliweweseka kimawazo na kushindwa kufanya uamuzi wa haraka,nilimtizama mtoto Jane alishindwa kuniangalia,mzozo uliendelea sasa haikuwa siri tena kwani sauti zilisikika kwa kila aliyekuwa karibu.
"Wewe kila siku unapanda boda boda ukitaka kwenda kazini na ukiwa unarudi mbona mimi sikuambii,unatumia shilingi elfu nne kila siku kwa ajili ya bodaboda ilhali ungeweza kutembea kwa miguu mpaka nyumbani si ungeweza kuokoa Laki moja na elfu ishirini (120,000/=) kwa mwezi?"Alihoji mkewe Shafii.
Umbali wa kutoka nyumbani mpaka barabarani ni mita mia mbili sawa na urefu wa viwanja viwili vya mpira.
Niliwaza juu ya hoja zao mbili ambazo zinaonekana dhahiri kuwa ni wivu wa matumizi mabaya ya pesa, nilipata jibu kuwa wote wana matumizi yasiyo ya lazima.
2: KUIGA TABIA ZISIZO NA MATOKEO MAZURI
Watu wengi hufanya kwa sababu wamemuona mtu flani anafanya,hivyo hupelekea kuishi maisha ya kuigiza kila siku,maisha haya hayana faida yeyote.Huwezi jua kwa nini yule anafanya hivyo yawezekana akawa na sababu ambazo wewe huzijui.
Mkasa wa Shafii na Mkewe uliendelea huku maskio yangu yakisikiliza kwa makini
"Nilishakuambia hao marafiki zako wanaokufundisha huu ujinga wa kuhudhuria kila harusi ya hapa mtaani sitaki kuwaona tena hapa nyumbani"Shafii alizungumza kwa hasira.
"Siwezi kuwaacha marafiki zangu nitaendelea kuwa nao na nitahudhuria sherehe kila napopata mwaliko,pesa ni ya kwangu,mshahara ni wangu halafu wewe unanipangia magumizi thubutuu"Ilikuwa ni sauti ya mke wa shafii ilisikika na kukatishwa ghafla.
"Hodi baba,baba mdogo amekuja" Jane alikuwa akimwita baba yake .
"Mkaribishe ndani"Baba yake alimjibu.
"Yupo amekaa kwenye kochi"Jane alimjibu baba yake huku akiusukuma mlango na kuingia chumbani kwa baba yake.
Shafii alitoka chumbani kwake na kuja sebureni,Sura yake ilijawa na aibu kiasi kwamba hata kunisalimu alipatwa na kigugumizi.
Nilimchangamkia ili niweze kundoa aibu aliyokuwanayo na niliyokuwanayo, Baada ya dakika tano kupita Shemeji(mkewe shafii) alikuja sebleni akiwa amefura na kifua kikiwa kimejaa hasira,hapo ndipo mambo yakawa hivi.(soma namba 4).
Ili uweze kufanikiwa ni lazima uachane na marafiki walio na fikra hasi juu ya maisha,wanaowaza kitchen party,vigodoro na mizimbao,walio na matumizi mabaya ya pesa,jiangalie wewe ulipo na unapokwenda kwani hakuna anayeweza kuubeba mzigo wako vijana wa siku hizi wanasema PAMBANA NA HALI YAKO.
4.KUTOKUWA NA BAJETI.
Bajeti ni muongozo wa matumizi ya pesa ambayo inakuwa imeandikwa katika karatasi,vifaa vya electronics n.k.Bila ya kuwa na bajeti kusingekuwa na mpangilio mzuri wa matumizi ya serikali,makampuni hata mtu binafsi.
Tunaendeshwa na bajeti ili kuweza kufikia malengo yetu tuliyojiwekea,kutokuwa na bajeti hatuwezi kufanya chochote wala malengo hatutayafikia.
Tukiwa tumekaa sebuleni walinieleza sababu ya ugomvi wao ambazo zililemea kwenye matumizi mabaya ya pesa katika mambo ambayo hayana umuhimu wala faida katika maisha yao.
Suala la bajeti ya pesa walizokuwa wanazikusanya lilikuwa ni shubiri kwao,kupelekea matumizi mabaya ya pesa na mara nyingine kukosa pesa ya chakula nyumbani na kusababisha madeni mengi na makubwa dukani kwa Mangi.
5. HISIA ZA KUPATA TENA KESHO
Hili ni suala ambalo watu wengi linawaathiri na athari zake zinakuja kuonekana hapo baadae,msemo wa tumia pesa ikuzoee umekuwa ni miongoni mwa misemo ambayo inaleta matokeo hasi katika maisha ya vijana wengi.
"Kwani shemeji nikipata mshahara wangu wa laki 5 kwa mwezi nikatumia laki 3 kwa ajili ya kununua nguo na mambo mengine,nikaweka laki 2 ya chakula nyumbani kuna ubaya gani?"Ilikuwa sauti ya Mke wa shafii ambaye alitaka ufafanuzi.
Swali hili limejengwa katika misingi ya "kesho nitapata hata kama nikitumia vibaya siku ya leo"Kitu ambacho ni sumu katika ustawi wa uchumi wa familia yako.
Pia maisha ya hawa wawili hayakuwa na mikakati kuhusu miaka 10 ijayo,bajeti zao zilikomea mwezi mmoja tena za kununua nguo za harusi.Maisha haya hautakiwi kuishi wewe unayesoma makala haya,Ishi maisha ya bajeti yenye matumizi mazuri ya pesa hapo ndipo utafikia uhuru kifedha.
Hadithi hii ni ya Kubuni haina ukweli wowote na majina yaliyotumika
Tembelea Blog Hii ya patamamboadress.blogspot.com
Mwandishi wa makala haya Bundala Izengo.0656669989
Jumatatu, 4 Septemba 2017
JE.NI SAHIHI KUCHAGULIWA KAZI/BIASAHARA YA KUFANYA?
Hili ni swali lililokosa majibu ya haraka baada ya kuulizwa na mdogo wangu ambae yuko chuo kikuu mwaka wa tatu hapa nchini Tanzania.
Nilihisi kama utani kumbe alikuwa akimaanisha na akitaka jibu sahihi na lenye muongozo katika hitaji lake la kujikimu kimaisha.
Swali hili lilinifanya nichakate akili na kujaribu kumweleza A na B nyeusi na nyeupe juu ya harakati za kutafuta maisha hasa kwake yeye ambaye bado ni mwanachuo.
Kijana huyu alikuwa na Wazo lake la biashara ambalo hakika analipenda na aliamini kuwa lingeweza kumfikisha kileleni kifedha na kujaribu kukidhi mahitaji yake muhimu.Kwa kuwa kijana huyu alikuwa bado yuko mikononi mwa wazazi ilimlazimu kuwashirikisha wazazi wazo lake,hapo ndipo alipokutana na vigingi.
"Baba nahitaji kufungua banda kwa ajili ya kuonyesha mpira"Ilikuwa ni sauti ya kijana huyu ambayo ilikuwa ikiomba ruhusa.
"Sawa lakini subiri kwanza tujadili na mama yako"Baba alimjibu huku akishangazwa na wazo la mwanae.
Saa zilipita na siku zikasogea bila ya kupata jibu la ombi lake.Aliamua kujaribu kumweleza mama yake
"Mama nina wazo la biashara ya kuonesha mpira kwani maeneo haya hakuna huduma hiyo hivyo vijana huenda kusini na mahariki ya jirani kutafuta huduma hiyo hasa wakati wa msimu wa mipira ya ulaya,ligi kuu Tanzania kombe la Afrika na dunia."Kijana huyu alizungumza na mama yake akimuomba apate ruhusa hiyo.
"Tumejadili na baba yako tumeona kuwa kuonyesha mpira unaweza kukusababishia kuharibika kimaadili kwa sababu wateja wako watavuta sigara,bangi,pombe na wengine kugombana hata kutukanana pia imani yetu hairuhusu ushabiki wa mpira,hivyo tumejadili na kuona kuwa sio vyema kukuruhusu kufanya biashara hiyo ambayo inamchukiza Mungu ni vyema uanzishe biashara ya kuchoma mahindi!"Alizungumza mama yake akisahau ya kuwa kijana wake ni shabiki damudamu wa Klabu ya mpira ya Man United na Simba.
"Daaahh sawa mama nimewasikia wazazi wangu"Ilikuwa ni ya sauti ya chini na huzuni ya kijana huyu ambaye ndoto zake ziliyeyuka mithiri ya barafu kwenye jua.
JE WAZAZI WALIKUWA SAHIHI KUMCHAGULIA KIJANA WAO KAZI BIASHARA?
Katika misingi ya mafanikio moja ya msingi wa mafanikio ni kufanya ukipendacho matharani hakivunji sheria za nchi,hicho ndicho kitakufikisha katika kilele kifedha,kulingana na jibu la wazazi wake alikata tamaa katika harakati zake za kutafuta maisha hivyo aliamua kunifuata kuniomba ushauri,kwani wazo la wazazi wake ilikuwa ni vigumu kulivuata kwa sababu hajawahi kulifanyia utafiti na wala hajawahi kufikilia kama siku moja atafanya biashara hiyo.
Sikuwa na hiana nilijaribu kumweleza mambo ambayo yanaweza kusababisha mtu kuchagua kazi.
1.SHERIA ZA NCHI
Kila nchi imetunga sheria zake kulingana na uhitaji wa sheria hizo kwa wanachi wake,mara nyingi sheria za nchi huwa hazibagui dini kabila wala utaifa Mfano.Ukibainika kuwa una kosa wewe ni mgeni katika nchi flani utahukumiwa kulingana na sheria za nchi hiyo.Hivyo basi ni vyema unapochagua wazo lako la biashara lisije likawa kinyume na sheria za nchi hiyo.Mfano Kenya ni ruhusa kutumia mirungi kwa ajili ya tiba,Tanzania ni kosa kubwa kutumia mirungi haijalishi kwa ajili ya tiba au biashara.Hivyo basi ukiangalia sheria za nchi hizi mbili zinakinzana ukitaka kufanya biashara hiyo ni bora ukahamia huko.
2.DINI
Hili ni tattizo kubwa sababu, dini zimekuwa zikichanganya waumini wake na kila kiongozi amekuwa akitafasiri mambo kulingana na yeye alivyoelewa,huwa nafikia wakati nasema ukisikiliza sana unaweza kuchanganyikiwa ukashindwa kufanya jambo lolote.Hawa wanasema Soda ni mbaya na hairuhusiwi kutumika kwa kinywaji, wengine wanaenda mbali zaidi wakipiga marufuku waumini wao kutumia baadhi ya vinywaji baridi wakifananisha majina ya vinywaji hivyo na madawa ya kilevya n.k
Ukweli ni kwamba miruzi hii inatupoteza mwelekeo, Mdogo wangu nakusihi fanya kile ukipendacho bila kuvunja sheria za nchi na maandiko ya Mungu wala sio fikra za watu.
3.MILA NA DESTUTI
Japokuwa sababu hizi zinaweza kuwa sababu za kizamani lakini bado kuna watu wanaendekeza Mila na Destuli katika kufanya kazi.Mila zimekuwa mwiba kwetu kwa sababu watu wamekuwa wakibagua kazi wakisema.
"Kazi hii ni ya mwanaume, na ile ni ya kike"Hizi ni sauti za watu ambao ni maskini wa mawazo,katika ulimwengu huu wa sayansi na technolojia uliochagizwa na ugumu wa maisha hakuna ubaguzi wa kazi wa namna hiyo Japokuwa bado watu wanafikra hizo.Miaka ya 199 - 2011 ilikuwa ni vigumu kukutana na konda mwanamke/Rubani wa ndege mwanamke lakini sasa hivi ni kawaida kuwaona akina dada wakichangamkia fulsa japokuwa jamii inaweza kukuchukulia katika mtizamo Chanya au Hasi.
4.MAZINGIRA.
Mazingira yanayotuzunguka yanaweza yakawa ni sababu ya kuchagua kazi,lakini pia mazingira haya haya yanawezakuwa fulsa kwetu hauwezi kufanya biashara ya kuuza barafu katika maeneo ya baridi kali hata kama unapenda biashara hiyo,lakini katika mazingira haya biashara ya kuuza kahawa na chai inalipa na chenji inabaki.
"Sawa kaka nimekuelewa"sauti ya mdogo wangu ilinifanya nikomee hapo na kuendelea kupiga soga nyingine zikiwa ni pamoja na kukagua mpango wake wa biashara ya kuonyesha mpira.Navyozungumza hiii leo amekuwa ni tegemezi nyumbani kwao.
Nimeandika haya ili nikutie moyo kijana mwenzagu usisikilize kelele za watu mbalimbali(akili za kuambiwa hanganya na zako),siku zote wanaoharibu mipango yako ni watu wa karibu yako.FANYA BIASHARA UIPENDAYO BILA KUVUNJA SHERIA ZA NCHI.
Nawatakia kazi njema Ni mimi Bundala .A. Izengo
Jumatano, 10 Mei 2017
“USIKU HUU WANAITAKA ROHO YANGU”
Sina ni binti aliyekuwa akiishi na na baba,mama pia bibi katika Kijiji cha Sengerema mkoani Mwanza baada ya dada zake wawili kufariki dunia katika mazingira ya kutatanisa.
Sina alimpenda sana kijana aliyejulikana kwa jina la Nipe, Nipe ni kijana aliyekuwa na sifa zote za kumwita mtanashati kwani alipendeza kwa kila aliyemtizama.
Ilikuwa ni vigumu kwa Sina kugundua siri nzito aliyokuwa nayo mama yake,kila kulipokucha mama yake alikuwa akibeba jembe na kwenda shambani hata kama wakati wa kiangazi.
Siku moja kulitokea Ngoma inayojulikana kwa jina la Chagolaga maarufu sana usukumani.
Sina na Nipe walihudhuria katika ngoma hiyo ambayo ilipambwa na vijana wa kisukuma waliokuwa wamejifunga lubega kwa shuka la rangi nyeusi,huku vifua vyao vilikuwa wazi na waliokuwa wakicheza mchezo wa kuchapana fimbo, mabinti wa kisukuma walijifunga kipande cha nguo nyeupe kilichokuwa kimefunika matiti na kilichokuwa kimezunguka na kufungwa mgongoni.
Ulifika wakati wa kuchagua mchumba ambapo mvulana alikwenda kumchagua binti wa kike ambaye alikuwa karidhika naye. Mchezo huu hugeuka kuwa sumu na kusababisha kifo pale vijana wa kisukuma wanapogongana kwa binti mmoja hivyo hupigana mpaka kuonekana mshindi.
Siku hiyo ilikuwa ni burudani ya kutosha katika kijiji cha Sengerema,kila mahali kulikuwa na kundi la watu waliokuwa wakishuhudia tukio hilo ambalo huwa ni la kijadi,hufungisha ndoa vijana wa kisukuma pasipo na mkono wowote wa baraka kutoka kwa Mwenyezi Mungu wala wazazi.
Ngoja nikupe dondoo za Ngoma hii; Ngoma hii huchezwa na vijana wa kabila la kisukuma hasa wakati wa mavuno, vijana wa kiume huchagua binti ambaye atakuwa naye usiku ule,kama akimpendeza huchukua hatua za kuoa,naomba tukomee hapo manake naweza kuchukua siku nzima kuelezea mabaya na mazuri katika ngoma hii.
Ilikuwa ni usiku wa saa tatu,Sina na Nipe walianza safari ya kurudi nyumbani, wakiwa njiani Sina alimwambia Nipe kuwa siku hiyo kuna kikao ambacho alihitajika kuhudhuria, aliendelea kumsihi kuwa asirudi nyumbani kwani kuna kitu kibaya kingemtokea hali ambayo angeweza kupoteza uhai.
Nipe alishangazwa sana na maneno, ambayo alishindwa kung'amua wala kutabiri killichotarajiwa kutokea usiku ule.
Alimwambia neno hilo kwa kumnong'oneza huku akimshika bega kwa msisitizo
"Usiku huu wanaitaka Roho yako".
“Unamaanisha nini mbona sikuelewi!”Nipe aliuliza kwa hamaki huku akiwa na shauku kubwa ya kujua ni kitu gani ambacho kingemtokea kama angelala nyumbani.
“Naomba unisikilize kwa makini mpenzi wangu Nipe. Mapenzi yangu kwako ni matamu kuliko hata sega la asali. Nakupenda sana ndiyo maana nakuomba usilale nyumbani."
"Kama utahitaji kuona basi twende katika mti ule wa ukwaju,ila ujue kuwa usiku huu wanaitaka roho yako.”
Ulikuwa ni usiku wa giza totoro,ulionakshiwa na manyunyu ya mvua na ngurumo za radi huku sauti za bundi zikisikika zikiashiria kuwa kulikuwa na kitu kibaya kilichokuwa kikiendelea.
Walisogea katika mti mkubwa wa ukwaju na kukaa chini Sina aliendelea kuzungumza.
“Nakupatia dawa hii jipake usoni”Sina alijipaka kama alivyoelekezwa
“Kisha panda juu ya mkwaju huu utakachokiona usishtuke kwani kutakuwa na kikao cha wachawi leo usiku nakuomba utulie kabisa kama unanyolewa”
Nipe alipanda juu ya mti wa mkwaju na kutulia kimya ambapo alimwacha Sina chini akikusanya mawe ambayo yalitumika kama mafiga ya kupikia.
Saa sita usiku iliwadia Nipe alikuwa juu ya mkwaju akipepesa macho kama kibaka aliyekuwa akimendea simu. Aliona fisi iliyokuwa akikimbia kwa kasi, mnyama huyo alifunga breki kali chini ya mti wa ukwaju, alipotizama kwa makini alimuona bibi kizee ambaye alikuwa ni jirani yake.
Bibi huyo alishuka kutoka juu ya Fisi huyo kwa staili ya aina yake, alitanguliza kichwa na kufuata kiwiliwili.
Haikupita hata sekunde kumi ziliingia Fisi mbili ambazo zilikuwa na mwendo mkali na kushusha wanaume wawili, haikuchelewa aliona fisi sita ambazo zilikuwa na ukubwa sawa na ndama nazo zilishusha akina mama na binti mdogo kabisa ambaye alimkadiria kuwa na miaka kumi na mitano.
Alipigwana butwaa alipomuona mama yake mzazi ambaye alikuja na usafiri huohuo na kushuka kwa staili hiyohiyo.
Nipe aliogopa sana moyo wake ulienda mbio hakuamini kabisa kama aliyemuona ni mama yake mzazi, alivuta picha ya nyumbani kwani kila siku mama yake hubeba jembe na kuelekea shambani kuchimba mizizi ya miti, alijikuta akiongea kwa sauti ya chini.
“Yawezekana mama akawa mchawi” Nipe aliendelea kutazama kilichokuwa kikiendelea chini ya Mkwaju huo.
Aliingia mkuu wa wachawi ambaye alikuwa akitokea Gamboshi iliyoko mkoani shinyanga wilayani Bariadi, kila mchawi alisimama na kuanza kupiga makofi kwa staili ya aina yake,walikunja mikono yao na kufanya kama kuku anayegonga mabawa akitaka kuwika.
Mkuu wa wachawi aliingia akiwa na ungo alitembea kwa kila aina ya madaha huku akifuatiwa na walinzi wake, alitokea mchawi mmoja ambaye alikuwa amebeba mtu ambaye Nipe alimfahamu.Alikuwa ni jirani yake ambaye ni mwenyekiti wa kijiji hicho,mama huyo alikuwa ni mnene na alikuwa na makalio makubwa. NIni kitaendelea endelea kufuatilia kupitia blog hii.
Jumamosi, 6 Mei 2017
ILIPOISHIA :-
Hakuna aliyekuwa akijua hata mmoja hali hizo kwani nyumbani walichukulia kama alikuwa mtu ambaye alipenda urembo na anayependa kuwasaidia watu wa hali ya chini hasa misikitni na makanisani.
ENDELEA
Watu wengi walimjua kuwa ni kijana mwenye roho nzuri aliyekuwa na kila aina ya huruma,mwenye kupenda watu na aliyekuwa akisaidia kwa hali na mali tena bila kinyongo chochote.
Baba alikuwa ni mtu mpole aliyekuwa mcheshi na aliyependa kulinda heshima yake kwa kuwapa watu salamu za upendo na amani.Alikuwa anakubalika kila alipokanyaga ama aliposimama kuzungumza, watu walimkubali na kumuona kuwa ni mtu mwenye hekima na busara, ni kijana ambaye a jasiri mwenye tama na pesa na aliweza kufanya lolote lile kwa ajiri ya kupata pesa.Ili kuthibitisha hayo msomaji tililika na ukurasa huu usifikiri nakupiga kabobo.
Siku moja tukiwa sebureni tunaangalia kituo kimoja cha Televisheni, mtangazaji wa zamu alitangaza tukio la vifo vya maalbino wawili huko mkoani Shinyanga hali ambayo watu wote tulikuwa kimya tukisikiliza habari hiyo iliyotikisa mtima wa kila mtanzania mpenda amani,lakini ilisikika sauti ya baba ikisema
“Aaa hivi unafikiri ningekuwa mimi ni mlemavu wa ngozi(albino)ningejikata mkono ili wanipe changu niendeleze maisha.”
Sauti hii iligonga kingo zaubongo wangu na kujikuta nikimtizama baba kwa jicho la kufikilia mengi juu yake,nilipiga picha ya kifikra na kugundua kuwa, Kama anashindwa kujihurumia mwenyewe je atamhurumia vipi mtu mwingine.
Ngoja nikupe angalizo kidogo msomaji….watu kama hawa hawaoni hatari kutoa kafara mama,baba,mtoto hata mkewe.Angalia usije ukaachana na mmeo kwa sababu ya kalamu yangu.
Kwa kuwa nilikuwa ni mchunguzi sana wa mambo mbalimbali ambayo baba alikuwa akiyafanya niliweza kugundua mengi juu ya siri ambayo alikuwanayo.
Nyumbani kulikuwa na nyumba tatu ambapo kulikuwa na nyumba moja kwa ajiri ya familia,nyumba hii ilikuwa na vyumba saba na sebule mbili,sebule ya kwanza ilikuwa ni sebure ambayo tuliitumia sisi (watoto).
Sebure ya pili ilikuwa ni sebure ambayo wageni wa kawaida walipumzika kama ndugu jamaa na marafiki,pembeni ya sebure hii kulikuwa na chumba cha kujisomea ambacho kilikuwa kimesheheni vitabu na kompyuta.
Pembezoni mwa chumba hiki kulikuwa na chumba kimoja kikubwa ambacho kikuwa kimesheheni kila aina ya starehe kama,bwawa la kuogelea,baa yenye kila kinywaji,video ya kuchezea gemu, sehemu zote zilijaa viyoyozi hali ambayo joto la Dar es salaamu lilikuwa ni hadithi kwetu.
Nyumba ya pili ilikuwa ni nyumba ambayo baba na mama walikuwa wakilala,nyumba hii ilikuwa ni ya vioo,haikujengwa kwa tofali wala simenti,ilikuwa na umbo la bikali Hakika ilipendeza kwa kila aliyeitizama.
Nyumba nyingine ilikuwa ni nyumba ya chini ambayo baba alikuwa amezuia mtu yeyote kuingia katika nyumba hii na baathi ya vyumba vilikuwa vimefungwa na funguo alikuwanayo mwenyewe.Katika lifti ya nyumba hii kulikuwa na alama ya nyoka na alama ya fuvu la kichwa.Namba za siri za kuingia katika lifti hii zilikuwa ni 666.
Namba hii 666 ni namba ya mpinga kristo ambayo ni namba inayotumiwa na freemasoni kuteka dunia kabla ya yesu kurudi mara ya pili.Haya nafikiri umenielewa manake ulishafikiri kuwa ni namba ya simu.
Ndani ya chumba hicho kulikuwa na alama mbalimbali ambazo wakati huo sikuzijua maana yake,si mimi tu hata mama,kaka wadogo zangu hawakuzijua.Tulizitizama alama hizo na kuziona kama mapambo mazuri yaliyonakshi kuta.
Pembeni ya chumba ambacho kilikuwa hakifunguliwi kulikuwa na viti viwili,na katikati ya viti hivyo kuliachanishwa na meza ambayo ilikuwa na alama zilizofanana na za ukutani zilizokuwa zimepangwa kwa ustadi mkubwa na kuifanya meza hiyo kupendeza vilivyo.
Katika chumba hiki kulikuwa na hewa nzuri kwan kulikuwa na mitambo maalumu ya kuingiza na kutoa hewa,chumba hiki kilikuwa kinatumika kwa wageni maalumu ambao baba alikuwa akiwapokea kutoka ndani na nje ya nchi.
Ndani ya chumba hiki kulikuwa na kifaa maalumu cha kusafisha nyumba,Chombo hiki kilifungwa na mafundi kutoka ujerumani.
Ngoja nikupe dondoo fupi kuhusu nyumba hii,ujenzi wa nyumba hii ilijengwa na mafundi kutoka Marekani,Afrika ya kusini na Nigeria.Mafundi hawa walijenga kwa awamu lakini cha kushangaza kila walipotaka kumalizia kujenga mmoja wao alifariki dunia kwa kupigwa na kitu kichwani ama kubanwa ama homa ya ghafla.Hiyo ndio historia fupi ya nyumba hii.
MDOGO WANGU KUTOLEWA KAFARA
Ilikuwa ni siku ya tatu ya juma ya mwezi wa 04 mwaka 2014 kabla ya sikukuu ya pasaka kufika,baba alitukalisha kikao cha familia ambapo tulizungumzia kuhusu kwenda kutalii katika moja ya mbuga za wanyama nchini Tanzania.
Ma zungumzo yetu yalikuwa na kila aina ya mabishano kwani baadhi yetu hawakutaka kwenda katika mbuga ambayo baba alikuwa akiitaja.Hali hii ilisababisha kuzua mtafaruko katika kikao hicho na kusababisha baba kutumia fimbo ya ukuu wa familia kulazimisha kukubali matakwa yake.
Hakuna aliyeweza kuzungumza tena baada ya baba kutoa tamko hilo ambapo aliamua kwenda kutembelea mbuga za wanyama za Serengeti.Tulipewa sikyu mbili za kujiandaa kwa kununua mavazi maalumu ya kuvaa mbugani na vyakula vya kusindika.
Mimi na wadogo zangu tulichukua gari letu na kwenda super market kufanya shoping hiyo,nyumbani kulikuwa na gari la baba,mama na magari mawili kwa ajiri ya watoto.
Baada ya kumaliza kufanya maandalizi hayo tulijiandaa kwa safari huku tukiwa na shangwe ya kwenda kuwaona sImba,Twiga na wanyamapori wengine.
Siku iliyofuata baba alipeleka gari lake kwa ajiri ya kufanyiwa matengenezo madogo madogo kwa kuliweka sawa na safari.Baba alirudi nyumbani,siku hiyo ilikuwa ni siku ya kipekee kwani baada ya kurudi nyumbani alifanya vitu viofuatavyo.
Aliingia katika nyumba ile ya chini na alikaa zaidi ya masaa mawili,sikuweza kujua kwa haraka alikuwa akifanya nini lakini ilinilazimu niingie ndani ya chumba hicho ili kukamilisha utafiti wangu.
Niliingia katika chumba cha liftio na kubofya 666 kisha lifti hiyo ilishuka chini na kunifikisha chini,nuilishuka na kuanza kupIga hatua kwa kunyata nikielekea katika chumba ambacho kilikuwa kinafungwa muda wote lakini wakati huo kilikuwa kimefunguliwa.
Hali ya nyumba ilikuwa kimya hali ya kwamba hata kama ukitoa pumzi ilisikika,nilisogea taratibu katika chumba hicho,mlango wa chumba hicho ulikuwa umeegesha huku ukiacha mpenyo mdogo ambao nilipitisha jicho langu na kutizama.
Nilimuona baba akiwa amevalia suti yake nyeusi ambayo ilikuwa iking’ara kama nyota ya mashariki,mkono wa kushoto alikuwa ameshikilia kitabu ambacho kilikuwa kimezungushiwa madini mbalimbali yaliyo na alama mbalimbali za mafuvu,vidole,nyoka na alama iliyofanana na umbo pweza.
Akiwa amekaza uso alikuwa akizungumza maneno ambayo sikuweza kuyang’amua mara moja lakini nilisikia neno la mwisho akimtaja mdogo wangu wa mwisho Chimo,kengere ya hatari ililia katika kichwa changu nilishindwa kuelewa mara moja kuhusu alichokuwa akikifanya.
Niliendelea kumtizama baba aliyekuwa akizungumza kwa hisia kali huku akiwa amefumba macho yake,ghafla nywele zangu zilisisimka na ubongo wangu ukapata taarifa kuwa kulikuwa kuna kitu kibaya kiliingia ndani.
Nilipiga moyo konde na kusema kuwa
“Nitaangalia mwanzo mpaka mwisho wa tukio hili”
Niliendelea kutizama tena kwa makini lakini nilishtuka nilipoona rangi ya taa hafifu zilizokuwa zikimulika ndani zikififia na kuwaka mwanga mkali ambao ulikuwa ukiwaka mfano wa radi,hali ambayo ilinifanya niumie macho na kushindwa kuona vizuri.
Nilitoa uso wangu katika kipenyo kile na kutizama kwingine…Haaa…!!!nilishangaa kuona nyumba yoye ilikuwa ikiwaka mwanga ambao nuilishindwa kuelewA ulikuwa ukitoka katika chanzo gain.
Nilianza kuutafuta mlango wa kutokea ambapo,nilishika lifti na kuingia kisha ilinitoa nje,ilikuwa imetimu saa sita usiku.Baada ya kutoka,nilielekea ndani na kuwakuta mama na wadogo zangu wawili wakijiuliza kuhusu kutoweka kwangu usiku huo.
Mama aliamini kuwa nilitoka na baba lakini wadogo zangu walikataa na kusema kuwa waliniona nikitoka peke yanu,nilishangaa sana kusikia kuwa hata mama hakujua baba alikoelekkea.
Nini kitaendelea endelea kufuatilia hadithi hii ya kusisimua.
Hakuna aliyekuwa akijua hata mmoja hali hizo kwani nyumbani walichukulia kama alikuwa mtu ambaye alipenda urembo na anayependa kuwasaidia watu wa hali ya chini hasa misikitni na makanisani.
ENDELEA
Watu wengi walimjua kuwa ni kijana mwenye roho nzuri aliyekuwa na kila aina ya huruma,mwenye kupenda watu na aliyekuwa akisaidia kwa hali na mali tena bila kinyongo chochote.
Baba alikuwa ni mtu mpole aliyekuwa mcheshi na aliyependa kulinda heshima yake kwa kuwapa watu salamu za upendo na amani.Alikuwa anakubalika kila alipokanyaga ama aliposimama kuzungumza, watu walimkubali na kumuona kuwa ni mtu mwenye hekima na busara, ni kijana ambaye a jasiri mwenye tama na pesa na aliweza kufanya lolote lile kwa ajiri ya kupata pesa.Ili kuthibitisha hayo msomaji tililika na ukurasa huu usifikiri nakupiga kabobo.
Siku moja tukiwa sebureni tunaangalia kituo kimoja cha Televisheni, mtangazaji wa zamu alitangaza tukio la vifo vya maalbino wawili huko mkoani Shinyanga hali ambayo watu wote tulikuwa kimya tukisikiliza habari hiyo iliyotikisa mtima wa kila mtanzania mpenda amani,lakini ilisikika sauti ya baba ikisema
“Aaa hivi unafikiri ningekuwa mimi ni mlemavu wa ngozi(albino)ningejikata mkono ili wanipe changu niendeleze maisha.”
Sauti hii iligonga kingo zaubongo wangu na kujikuta nikimtizama baba kwa jicho la kufikilia mengi juu yake,nilipiga picha ya kifikra na kugundua kuwa, Kama anashindwa kujihurumia mwenyewe je atamhurumia vipi mtu mwingine.
Ngoja nikupe angalizo kidogo msomaji….watu kama hawa hawaoni hatari kutoa kafara mama,baba,mtoto hata mkewe.Angalia usije ukaachana na mmeo kwa sababu ya kalamu yangu.
Kwa kuwa nilikuwa ni mchunguzi sana wa mambo mbalimbali ambayo baba alikuwa akiyafanya niliweza kugundua mengi juu ya siri ambayo alikuwanayo.
Nyumbani kulikuwa na nyumba tatu ambapo kulikuwa na nyumba moja kwa ajiri ya familia,nyumba hii ilikuwa na vyumba saba na sebule mbili,sebule ya kwanza ilikuwa ni sebure ambayo tuliitumia sisi (watoto).
Sebure ya pili ilikuwa ni sebure ambayo wageni wa kawaida walipumzika kama ndugu jamaa na marafiki,pembeni ya sebure hii kulikuwa na chumba cha kujisomea ambacho kilikuwa kimesheheni vitabu na kompyuta.
Pembezoni mwa chumba hiki kulikuwa na chumba kimoja kikubwa ambacho kikuwa kimesheheni kila aina ya starehe kama,bwawa la kuogelea,baa yenye kila kinywaji,video ya kuchezea gemu, sehemu zote zilijaa viyoyozi hali ambayo joto la Dar es salaamu lilikuwa ni hadithi kwetu.
Nyumba ya pili ilikuwa ni nyumba ambayo baba na mama walikuwa wakilala,nyumba hii ilikuwa ni ya vioo,haikujengwa kwa tofali wala simenti,ilikuwa na umbo la bikali Hakika ilipendeza kwa kila aliyeitizama.
Nyumba nyingine ilikuwa ni nyumba ya chini ambayo baba alikuwa amezuia mtu yeyote kuingia katika nyumba hii na baathi ya vyumba vilikuwa vimefungwa na funguo alikuwanayo mwenyewe.Katika lifti ya nyumba hii kulikuwa na alama ya nyoka na alama ya fuvu la kichwa.Namba za siri za kuingia katika lifti hii zilikuwa ni 666.
Namba hii 666 ni namba ya mpinga kristo ambayo ni namba inayotumiwa na freemasoni kuteka dunia kabla ya yesu kurudi mara ya pili.Haya nafikiri umenielewa manake ulishafikiri kuwa ni namba ya simu.
Ndani ya chumba hicho kulikuwa na alama mbalimbali ambazo wakati huo sikuzijua maana yake,si mimi tu hata mama,kaka wadogo zangu hawakuzijua.Tulizitizama alama hizo na kuziona kama mapambo mazuri yaliyonakshi kuta.
Pembeni ya chumba ambacho kilikuwa hakifunguliwi kulikuwa na viti viwili,na katikati ya viti hivyo kuliachanishwa na meza ambayo ilikuwa na alama zilizofanana na za ukutani zilizokuwa zimepangwa kwa ustadi mkubwa na kuifanya meza hiyo kupendeza vilivyo.
Katika chumba hiki kulikuwa na hewa nzuri kwan kulikuwa na mitambo maalumu ya kuingiza na kutoa hewa,chumba hiki kilikuwa kinatumika kwa wageni maalumu ambao baba alikuwa akiwapokea kutoka ndani na nje ya nchi.
Ndani ya chumba hiki kulikuwa na kifaa maalumu cha kusafisha nyumba,Chombo hiki kilifungwa na mafundi kutoka ujerumani.
Ngoja nikupe dondoo fupi kuhusu nyumba hii,ujenzi wa nyumba hii ilijengwa na mafundi kutoka Marekani,Afrika ya kusini na Nigeria.Mafundi hawa walijenga kwa awamu lakini cha kushangaza kila walipotaka kumalizia kujenga mmoja wao alifariki dunia kwa kupigwa na kitu kichwani ama kubanwa ama homa ya ghafla.Hiyo ndio historia fupi ya nyumba hii.
MDOGO WANGU KUTOLEWA KAFARA
Ilikuwa ni siku ya tatu ya juma ya mwezi wa 04 mwaka 2014 kabla ya sikukuu ya pasaka kufika,baba alitukalisha kikao cha familia ambapo tulizungumzia kuhusu kwenda kutalii katika moja ya mbuga za wanyama nchini Tanzania.
Ma zungumzo yetu yalikuwa na kila aina ya mabishano kwani baadhi yetu hawakutaka kwenda katika mbuga ambayo baba alikuwa akiitaja.Hali hii ilisababisha kuzua mtafaruko katika kikao hicho na kusababisha baba kutumia fimbo ya ukuu wa familia kulazimisha kukubali matakwa yake.
Hakuna aliyeweza kuzungumza tena baada ya baba kutoa tamko hilo ambapo aliamua kwenda kutembelea mbuga za wanyama za Serengeti.Tulipewa sikyu mbili za kujiandaa kwa kununua mavazi maalumu ya kuvaa mbugani na vyakula vya kusindika.
Mimi na wadogo zangu tulichukua gari letu na kwenda super market kufanya shoping hiyo,nyumbani kulikuwa na gari la baba,mama na magari mawili kwa ajiri ya watoto.
Baada ya kumaliza kufanya maandalizi hayo tulijiandaa kwa safari huku tukiwa na shangwe ya kwenda kuwaona sImba,Twiga na wanyamapori wengine.
Siku iliyofuata baba alipeleka gari lake kwa ajiri ya kufanyiwa matengenezo madogo madogo kwa kuliweka sawa na safari.Baba alirudi nyumbani,siku hiyo ilikuwa ni siku ya kipekee kwani baada ya kurudi nyumbani alifanya vitu viofuatavyo.
Aliingia katika nyumba ile ya chini na alikaa zaidi ya masaa mawili,sikuweza kujua kwa haraka alikuwa akifanya nini lakini ilinilazimu niingie ndani ya chumba hicho ili kukamilisha utafiti wangu.
Niliingia katika chumba cha liftio na kubofya 666 kisha lifti hiyo ilishuka chini na kunifikisha chini,nuilishuka na kuanza kupIga hatua kwa kunyata nikielekea katika chumba ambacho kilikuwa kinafungwa muda wote lakini wakati huo kilikuwa kimefunguliwa.
Hali ya nyumba ilikuwa kimya hali ya kwamba hata kama ukitoa pumzi ilisikika,nilisogea taratibu katika chumba hicho,mlango wa chumba hicho ulikuwa umeegesha huku ukiacha mpenyo mdogo ambao nilipitisha jicho langu na kutizama.
Nilimuona baba akiwa amevalia suti yake nyeusi ambayo ilikuwa iking’ara kama nyota ya mashariki,mkono wa kushoto alikuwa ameshikilia kitabu ambacho kilikuwa kimezungushiwa madini mbalimbali yaliyo na alama mbalimbali za mafuvu,vidole,nyoka na alama iliyofanana na umbo pweza.
Akiwa amekaza uso alikuwa akizungumza maneno ambayo sikuweza kuyang’amua mara moja lakini nilisikia neno la mwisho akimtaja mdogo wangu wa mwisho Chimo,kengere ya hatari ililia katika kichwa changu nilishindwa kuelewa mara moja kuhusu alichokuwa akikifanya.
Niliendelea kumtizama baba aliyekuwa akizungumza kwa hisia kali huku akiwa amefumba macho yake,ghafla nywele zangu zilisisimka na ubongo wangu ukapata taarifa kuwa kulikuwa kuna kitu kibaya kiliingia ndani.
Nilipiga moyo konde na kusema kuwa
“Nitaangalia mwanzo mpaka mwisho wa tukio hili”
Niliendelea kutizama tena kwa makini lakini nilishtuka nilipoona rangi ya taa hafifu zilizokuwa zikimulika ndani zikififia na kuwaka mwanga mkali ambao ulikuwa ukiwaka mfano wa radi,hali ambayo ilinifanya niumie macho na kushindwa kuona vizuri.
Nilitoa uso wangu katika kipenyo kile na kutizama kwingine…Haaa…!!!nilishangaa kuona nyumba yoye ilikuwa ikiwaka mwanga ambao nuilishindwa kuelewA ulikuwa ukitoka katika chanzo gain.
Nilianza kuutafuta mlango wa kutokea ambapo,nilishika lifti na kuingia kisha ilinitoa nje,ilikuwa imetimu saa sita usiku.Baada ya kutoka,nilielekea ndani na kuwakuta mama na wadogo zangu wawili wakijiuliza kuhusu kutoweka kwangu usiku huo.
Mama aliamini kuwa nilitoka na baba lakini wadogo zangu walikataa na kusema kuwa waliniona nikitoka peke yanu,nilishangaa sana kusikia kuwa hata mama hakujua baba alikoelekkea.
Nini kitaendelea endelea kufuatilia hadithi hii ya kusisimua.
Alhamisi, 4 Mei 2017
BABA USINITOE KAFARA KWA FREEMASON
Maisha ya nyumbani yalibadilika ghafla,yalikuwa ni maisha mazuri ambayo yalifanana kabisa na maisha ya kuzimu,vizimbao na matanuzi ya hapa na pale yalitawala maisha yetu ambapo kila mwaka tulikuwa tunachagua sehemu ya kwenda kupumzika.
Baba yangu alikuwa ni tajiri wa kutupwa na alikuwa akizidi kupata pesa nyingi ambazo hatukujua zilikuwa zinatoka wapi.Maswali mengi tulijiuliza vichwani mwetu
“Je ni kile kibanda cha kuchomea chipsi ndicho kinachomwingizia baba pesa nyingi kiasi hiki hali ambayo amekuwa ni tajiri wa kutisha kiasi hiki?”
Kwa kuwa nilikuwa ni mdogo sikuwaza wala kuthubutu kuuliza uhalali wa baba kumiliki pesa mali hizo nyingi.Maisha yetu yalikuwa ni ya kula baga,pizza na kutembelea magari ya kifahari.
Baba aliweza kuchinja ng’ombe kila ijumaa ya mwisho wa mwezi lakini akija mgeni asichinjiwe hata kuku.Hakuna aliyekuwa akijua siri nzito aliyokuwanayo baba yangu ambaye aliitwa kwa jina linalopendwa na watu wengi duniani ‘Mapesa’.
Cha kushangaza kila alipotaka kuchinga Ng’ombe alitufukuza nyumbani ama alitupa pesa kwa ajiri ya kwenda kubarizi ufukweni au kuingia katika kumbi za starehe.Alikuwa akibaki yeye peke yake nyumbani hata mama pia alimficha.
Kila ijumaa ya mwisho wa mwezi tulikuta nyama nyingi na ngozi ya ng’ombe ambayo hugawia maskini,makanisani na misikitini huku bila ya kuibakisha hata mnofu mmoja kwa ajiri ya nyumbani.Mara nyingi alipokuwa akichinja ng’ombe alikuwa akiagiza nyama nyingine kutoka buchani kwa ajiri ya matumizi ya nyumbani.
Alikuwa akipokelea mkono wa kushoto unapompatia pesa ama anapotoa pesa ,alikuwa akiutumia mkono wa kushoto katika kubeba begi lenye pesa na kuchukua ama kuvuata droo iliyokuwa na pesa.
Ngoja nikumegulie siri kidogo,mkono wa kushoto ni mkono autumiao shetani katika kutimiza haja zao,Luthifa ambaye ndiye mkuu wa freemasoni anatumia mkono wa kushoto katiaka kuwaapisha ama kupokea kitu..haya endelea kutililika.
Siku ya kuchinja ng’ombe alikuwa anavaa suti nyeusi iliyotengenezwa kwa madini ya ajabu ambayo sijawahi kuyaoni,na kuifanya suti hiyo kung’ra kuliko kitu chochote duniani.Pete aliyokuwa anavaa siku hiyo ilikuwa ni pete ya ajabu ambayo ilikuwa na alama ya fuvu na joka kubwa ambalo lilifanana na samaki aina ya pweza.
Pia alikuwa na cheni ya shingoni ambayo ilikuwa nakila aina ya madini na ailiyokuwa iking’ara katika kiza na iliyokuwa na chata ya vidole viwili.Kila alipokuwa akizungumza na watu alikuwa akishika kimoja kati ya hivyo.
Katika uchunguzi wangu wa kila siku kuhusu baba sikuwahi kumuona amevaa nguo ya ndani(chupi)hata kwa bahati mbaya.Heee….najua utaujiuliza nilikuwa namuona vipi.
Baba alikuwa na umbo kubwa hivyo kutokana na umbo lake ilikuwa ni virahisi kujua kama alikua amevaa kitu ama la.
Hakuna aliyekuwa akijua hata mmoja hali hizo kwani nyumbani walichukulia kama alikuwa mtu ambaye alipenda urembo na anayependa kuwasaidia watu wa hali ya chini hasa misikitni na makanisani.
Watu wengi walikuwa wakimjua kuwa alikuwa ni kijana mwenye roho nzuri aliyekuwa na kila aina ya huruma,mwenye kupenda watu na aliyekuwa akisaidia kwa hali na mali tena bila kinyongo chochote.
Baba alikuwa ni mtu mpole, mcheshi aliyependa kulinda heshima yake kwa kuwapa watu salamu za upendo na amani.Alikubalika kila alipokanyaga ama aliposimama kuzungumza watu walimkubali na kumuona kuwa ni mtu mwenye hekima na busara.
Baba alikuwa ni kijana ambaye alikuwa jasiri mwenye tamaa na pesa na aliweza kufanya lolote lile kwa ajiri ya kupata pesa.Ili kuthibitisha hayo msomaji tililika na ukurasa huu usifikiri nakupiga kabobo.
Siku moja tukiwa sebureni tunaangalia kituo kimoja cha Televisheni mtangazaji wa zamu alitangaza tukio la vifo vya maalbino wawili huko mkoani Shinyanga hali ambayo watu wote tulikuwa kimya tukisikiliza habari hiyo,lakini ilisikika sauti ya baba ikisema
“Aaa hivi unafikiri ningekuwa mimi ni mlemavu wa ngozi(albino)ningejikata mkono ili wanipe changu niendeleze maisha.”
Sauti hii iligonga kingo za kichwa changu na kujikuta nikimtizama baba kwa jicho la kufikilia mengi juu yake na nilipiga picha na kugundua kuwa Kama anashindwa kujihurumia mwenyewe je atamhurumia vipi mtu mwingine.
Ngoja nikupe angalizo kidogo msomaji….watu kama hawa hawaoni hatari kutoa kafara mama,baba,mtoto hata mkewe.Angalia usije ukaachana na mmeo kwa sababu ya kalamu yangu cha kuzingatia fanya uchunguzi wa kutosha.
Kwa kuwa nilikuwa ni mchunguzi sana wa mambo mbalimbali ambayo baba alikuwa akiyafanya niliweza kugundua mengi juu ya siri ambayo alikuwanayo.
Nyumbani kulikuwa na nyumba tatu ambapo kulikuwa na nyumba moja kwa ajiri ya familia,nyumba hii ilikuwa na vyumba saba na sebule mbili,sebule ya kwanza ilikuwa ni sebure ambayo tuliitumia sisi.
Sebure ya pili ilikuwa ni sebure ambayo wageni wa kawaida walipumzika kama ndugu jamaa na marafiki,pembeni ya sebure hii kulikuwa na chumba cha kujisomea ambacho kilikuwa kimesheheni vitabu na kompyuta.
Pembeni ya chumba hiki kulikuwa na chumba kimoja kikubwa ambacho kilikuwa kimesheheni kila aina ya starehe kama,bwawa la kuogelea,baa yenye kila kinywaji,video ya kuchezea gemu, sehemu zote zilijaa viyoyozi hali ambayo joto la Dar es salaamu lilikuwa ni hadithi kwetu.
Nyumba ya pili ilikuwa ni nyumba ambayo baba na mama walikuwa wakilala,nyumba hii ilikuwa ni ya vioo,haikujengwa kwa tofali wala simenti,ilikuwa na umbo la uyoga Hakika ilipendeza kwa kila aliyeitizama. Nini kitaendelea tembelea Blog hii ili kujua yatakayojiri.
Ijumaa, 27 Januari 2017
HAYA NDIO MAAJABU YA CHUNGWA
Chungwa ni tunda linalostawi ulimwenguni kote , lakini haswa tunda hili lilianza kusini mwa bara la Asia, huku likilimwa sana huko nchini China.
Chungwa lina kiwango cha juu cha vitamin C, huku nyama /ngozi nyeupe iliyozunguka kati ya ngozi ya nje na tunda lililomenywa ni chanzo kizuri cha madini ya ‘calcium.’
Mtaalam wa tiba asili kutoka Mandai Herbalist Clinic, Dk Abdallah Mandai anasema kuwa kwa wale wanaosumbuliwa na mafua wanaweza kuongeza maji ya moto katika juisi ya chungwa kisha mhusika anywe.
Mtaalam huyo, anaeleza kuwa majani ya mchungwa yakipondwa na kisha kuchanganywa na maji ya moto pamoja na asali kidogo, kwa ujumla mchanganyiko huo hutumika kama dawa ya kikohozi.
Aidha, Dk Mandai anafafanua kuwa endapo maua makavu yakisagwa nakuchanganywa katika maji ya moto ni dawa ya shinikizo la mishipa ya fahamu. Huku maganda yake yakisuguliwa usoni huwa ni dawa ya chunusi.
Pamoja na hayo, Dk Mandai anabainisha kuwa kwa ujumla juisi ya machungwa husaidia ugonjwa wa pumu, matatizo ya kifua, kusafisha damu, kupooza, kuungua, matatizo ya meno pamoja na beriberi.
.
Mbali na magonjwa hayo, pia husaidia matatizo ya kizazi, mishipa ya damu, magonjwa ya ngozi, matatizo ya mirija ya uzazi, husaidia usagaji wa chakula mwulini pamoja na kutuliza kichefuchefu kwa wajawazito.
Hizo ndizo baadhi ya dondoo muhumu za faida za machungwa kwa afya
TEMBELEA BLOG HII KILA SIKU UPATE MAMBO MENGI YANAYOHUSU AFYA NA UREMBO
Alhamisi, 26 Januari 2017
UKISTAAJABU YA MAFUTA YA NAZI UTAYAONA YA TUI LA NAZI
1. Mafuta ya nazi kwa afya ya MoyoMafuta ya nazi yana asidi mhimu sana kwa afya ya moyo iitwayo ‘lauric acid’ ambayo ina uwezo mkubwa kuuweka moyo wako katika hali ya afya na furaha kwa kuidhibiti kolesteroli/lehemu mbaya katika moyo na mwili kwa ujumla. Lauric acid huongeza uwepo wa kolesteroli nzuri mwilini ijulikanayo kwa kitaalamu kama High Density Lipoprotein (HDL) huku ikiishusha ile kolesteroli mbaya ijulikanayo pia kwa kitaalamu kama Low Density Lipoprotein (LDL) jambo ambalo ni mhimu kwa afya ya moyo kama anavyosema Lovisa Nilsson, mtaalamu wa lishe wa Lifesum.
2. Mafuta ya nazi huuongezea nguvu mfumo wa mmeng’enyo wa chakulaHii ndiyo moja ya faida ya mafuta ya nazi niipendayo zaidi. Ndiyo mafuta ya nazi yanayo uwezo kusaidia kudhibiti uzito uliozidi kwa sababu mafuta haya ni mepesi kumeng’enywa na hayagandi kama yalivyo mafuta mengine mazito (fatty acids) jambo linalosaidia kuuondoa uzito uliozidi mwilini. Kutokana na kitendo hiki cha kuongeza uwezo wa mwili kukimeng’enya chakula, watu wanaoyatumia mafuta haya kupikia vyakula vyao kila siku kwa kawaida huwa na uzito wa kawaida. Anasema Geeta Sidhu Robb, mtaalamu wa lishe na mwanzilishi wa Nosh Detox.
3. Mafuta ya nazi hung’arisha ngoziSiyo sehemu za ndani tu ya mwili zinazofaidika na mafuta haya ya nazi kama yanavyofanya mafuta mengine ya asili, kama unataka kuwa na ngozi nzuri yenye mng’aro na yenye afya na yenye muonekano wa asili basi paka mafuta ya nazi kila siku kwenye ngozi yako, mafuta ya nazi yana uwezo mkubwa katika kuua bakteria, virusi, na vijidudu vya aina yeyote vinavyoweza kuidhuru ngozi, haya ni mafuta kwa mwili mzima yaani pakaa kwenye ngozi yote usoni, mwilini, kwenye nywele na kwenye kucha. Pia unaruhusiwa kuyatumia mafuta haya wakati wa masaji.
4. Huongeza nguvu mwiliniMafuta ya nazi ni chanzo kizuri cha nguvu ya mwili kwani yana sifa ya kuelea kwa kiasi kidogo kwenye damu ‘medium chain triglycerides – MCT’ ambapo sifa hii huyafanya kusafirishwa moja kwa moja hadi kwenye ini ambako hutumika kama chanzo cha haraka cha nguvu au hubadililishwa kuwa ‘ketones’ ambacho ni chakula cha ubongo. Kwahiyo ikiwa unatafuta lift ya kuinua nguvu yako basi chukua kijiko kimoja cha chai cha mafuta ya nazi weka kwenye kikombe chako cha juisi au uji na utaona maajabu.
5. Ni mafuta mubadala ya kupikia yenye afyaTofauti na mafuta ya alizeti au hata mafuta ya zeituni, kupika chakula kwa mafuta ya nazi ni zaidi ya afya. Mafuta haya yana uwezo mkubwa wa kuungua na bado yakabaki na viinilishe vyake kama kawaida hata baada ya kuunguzwa au kuchomwa katika moto, hii ni kwamba mafuta kama ya zeituni ambayo huweza kuliwa hata yakiwa mabichi lakini yanapochomwa katika moto basi ubora wake hupungua au kwa maneno mengine huzalisha taka sumu kama ilivyo kwa vitu vingi vinapounguzwa lakini hili halitokei kwa mafuta ya nazi!
6. Ni mafuta mazuri kwa wasiopenda kutumia mafuta yatokanayo na wanyamaSiyo kupika tu na mafuta ya nazi ndiko huleta afya, bali pia ni mafuta mazuri kwa wasiopenda kutumia mafuta yatokanayo na wanyama kama mubadala kwa siagi au vitu vingine mnavyopaka juu ya mikate mnapokula. Hii nikwa sababu mafuta ya nazi hubaki kuwa magumu hata katika joto la kawaida la chumba tofauti na mafuta mengine.
7. Huzuia maradhi mengi hatari mwiliniKama ilivyo katika kuipunguza kolesteroli, mafuta ya nazi yanao uwezo mkubwa katika kuzuia na kutibu magonjwa mengine sababu ya kuwa na kiasi kingi cha asidi iitwayo lauric acid.Utafiti mwingi umeendelea kuthibitisha kuwa hii lauric asidi hubadilishwa kuwa asidi mafuta nyingine ijulikanayo kwa kitaalamu kama ‘monolaurin’ ambayo inayo sifa ya kudhibit na kuvizuia baadhi ya virusi ikiwemo vile vya ukimwi kuziingia na kuzidhuru seli za mwili na kusababisha maradhi mwilini. Ili kutibu virusi vya ukimwi inashauriwa kunywa glasi 4 za tui la nazi kila siku kwa muda wa miezi mitatu mpaka minne na utaona maajabu.
8. Hutibu tatizo la kupoteza kumbukumbuHii inaweza ikakushangaza kidogo unapoisikia kwa mara ya kwanza lakini tafiti nyingi zimeonyesha kuwa mafuta ya nazi yanao uwezo kuziamusha seli na shughuli za ubongo na katika kufanya hivyo kutasaidia kuzuia matatizo ya uwendawazimu au ukichaa (dementia) na kupoteza kumbukumbu (Alzheimer).
9. Hutumika kulainisha uke mkavuMafuta ya nazi yana matumizi mengi sana mwilini zaidi ya 100, kuna wanawake wana tatizo la kuwa na uke mkavu muda wote hata wakisisimuliwa vipi bado huwa wakavu, kuondokana na tatizo hilo pakaa mafuta ya nazi katika uke wako na utaona faida yake tena bila madhara yeyote hasi.
10. Husaidia katika ugonjwa wa alejiTukisema tuelezee faida zote za mafuta ya nazi kwa hakika hatutaweza, moja ya faida zake zinazoshangaza wengi ni uwezo wa kudhibiti dalili za ugonjwa wa aleji, kila siku pakaa mafuta ya nazi ndani ya pua zako na uone kama utapiga chafya unapokuwa karibu na kile kinachokuletea aleji/mzio.MHIMU:Hakikisha unapata mafuta ya nazi ambayo ni ya asili kwa asilimia 100, ikiwa utanunua dukani kuna uwezekano mkubwa yakawa yamechanganywa na kemikali zingine au haidrogeni kitu kinachoyapunguzia thamani ile ya asili. Kama unapikia kwenye chakula najuwa wengi mnapenda wali wa nazi au hata tui lake likiwekwa kwenye samaki au hata mboga yoyote lazima utajing’ata ulimi, basi nakushauri usichanganye na mafuta mengine kwenye hicho chakula.
Ijumaa, 28 Oktoba 2016
MWANAUME MWENYE MALENGO NA WEWE UTAMTAMBUA KWA HAYA
Nimekuwekea hapa zisome Tabia za mwanaume mwenye malengo na wewe.
1. Anakupigia simu mara kwa mara na kukuuliza siku yako imeendaje. Anafanya hivi kirafiki na kwa upendo, haigizi. Anakupenda kweli.
2. Anakutembelea mara kwa mara, anakuwa karibu na wewe kipindi unaumwa, hii inamaanisha kwamba yupo tayari kukuvumilia katika shida na raha. Mpende mwanaume huyu.
3. Anawapenda ndugu zako kama ndugu zake. Anaongea nao vizuri na kusaidiana mambo ya hapa na pale. Mtizame kwa jicho la tatu huyu mwanaume!
4. Anaongea na wewe kwa adabu na kwa upole, anakukosoa bila wasiwasi kama kuna mambo unaenenda visivyo. Anakuelekeza njia zilizonyoka..sio wa kumuacha huyu!
5. Hakulazimishi kufanya mapenzi. Anakupenda sana kiasi kwamba hawezi kukulazimisha jambo ambalo hauko na hiari nalo. Yupo karibu na wewe wakati wote na sio tu anapokutaka kimapenzi, huyu ni bonge la bwana.
6. Anakusaidia fedha pale unapokua umekwama kabisa, yuko na jukumu la kukusaidia kiuchumi. Anapenda kukupa kile ambacho amejaaliwa nacho. Hana mkono wa birika, Huyu anakupenda!
7. Anazungumzia future yake na wewe, mipango ya baadae pamoja na wewe, huyu anayo dhamira ya dhati kutoka moyoni mwake ya kukufanya uwe mkewe.
Hizi ni moja ya dalili kwamba mwanaume wako anakupenda na anataka atengeneze future pamoja na wewe. Usikate tamaa juu ya mwanaume wa aina hii.
Hao wenye sixpack sijui eight pack, wabeba vyuma, wavaa milegezo, wanyonya midomo na mahandsome wavaa hereni, waume za watu, masupa staa, watoto wa vigogo, hawatakusaidia lolote, utabaki ukiumizwa tu moyo wako.
Kabla hujajipendekeza kwa wanaume wa aina hiyo, jiulize wanawake wanzako wangapi wameshajipendekeza kwa sababu ya hzo pesa zake, hivyo na wewe unajiongeza kwenye foleni!
Mvumilie mwanaume wako, anazo ndoto njema, mapenzi ya kweli ni vigumu sana kuyapata. Ila pesa na mali ni rahisi sana kuzipata kama utajibidiisha.
Usipende mitelemko, mitelemko mingine ni njia ziletazo mauti! - Ukishikwa shikamana, ukipendwa, pendeka!
"Don't date a rich man, date a GOOD MAN, Good man will spend his life trying to keep u happy, no rich man can buy that!"
TANESCO YAIDAI SERIKALI MABILIONI
Na SARAH MOSES, DODOMA
SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco), limeiambia Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), kwamba linaidai Serikali zaidi ya Sh bilioni 125 kutokana na huduma za umeme linazotoa katika taasisi za umma pamoja na Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO).
Hayo yalielezwa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Felchesmi Mramba, wakati akijibu hoja za wajumbe wa kamati hiyo waliotaka kujua juu ya ripoti ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) inayoishia Juni 2015 kuhusu hesabu za shirika hilo.
Akiendelea kufafanua kuhusu hoja hiyo ya madeni, Mramba alisema tayari shirika hilo limeanza kufanya mikutano kadhaa na ZECO kwa ajili ya kuweka mikakati itakayofanikisha deni hilo la tangu mwaka 2013, kulipwa.
“Katika mikutano ile, tulibaini kuwa ZECO inashindwa kulipa kwa sababu inatoza gharama ndogo kwa watumiaji wa umeme Zanzibar tofauti na gharama za ununuaji umeme kutoka Tanesco,”alisema Mramba.
Kuhusu mikakati iliyoanza kuchukuliwa na shirika hilo ili kukabiliana na hali hiyo, Mramba alisema kwa sasa wameanza kuondoa mita zote za kawaida na kuweka mita za LUKU.
“Katika hilo, hadi sasa tumefanikiwa kuondoa mita za kawaida kwa takribani asilimia 99 kwa wateja wa kawaida ikiwa ni pamoja na kufungia taasisi kubwa za Serikali kama vile polisi, Jeshi la Wananchi wa Tanzania na Jeshi la Magereza.
“Hili la Luku, tunatarajia hadi Aprili mwakani, tutakuwa tumelikamilisha kwa taasisi zote za Serikali,” alisema Mramba.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya PAC, Naghejwa Kaboyoka, aliiagiza Serikali ihakikishe inalipa madeni hayo ndani ya miezi sita.
“Ni wakati sasa shirika hilo liachwe lijiendeshe lenyewe kibiashara kwani kwa hali ya sasa ilivyo, haileti maana mwananchi wa kawaida abanwe ili alipie bili yake ya umeme, wakati taasisi kubwa za Serikali zikiachwa na mlundikano wa madeni wa bili hizo za umeme,”alisema Kaboyoka.
Source: Mtanzania
Alhamisi, 27 Oktoba 2016
TAJIRIKA:NA UFUGAJI WA KUKU
Hebu anza na kuku Watano (5) tu Majike wenye Rika/Umri mmoja (au wanaokaribiana).
Watunze vizuri kwa kuwapatia chakula kilicho na mchanganyiko kamili wa viini lishe
vinavyotakiwa katika mwili wa kuku,
yaani;
wanga, protini, calcium, chumvichumvi, madini joto nk (kama nilivyoeleza hapa chini). Wawekee na Jogoo mmoja mzuri wa kienyeji/ kizungu/chotara (kama nilivyoeleza hapa chini juu ya uchaguzi wa majogoo).
Wanapoanza kutaga watayarishie mahali pazuri/Kiota kizuri cha kutagia na kuatamia kwa kuwajengea viota ndani ya banda.
Hakikisha mahali hapo hapavuji wala hapapati unyevunyevu wala joto kali sana. Hakikisha mahali hapo pana usalama wa kutosha (mahali wanyama hatari kama vicheche, pakashume, nyoka nk hawawezi kufika).
Kuku wakiendelea kutaga na sasa ukaona wanakaribia kuatamia,Anza kuchagua aina ya mayai unayotaka kuku wako walalie. Hii inamaanisha kuwa; ukichagua mayai makubwamakubwa hayo yanakuwa na vifaranga majogoo na mayai madogomadogo mara nyingi huwa ni ya vifaranga majike.
Acha kuwawekea mayai ya mviringo kama mpira!
Hakikisha kuku wote wanasubiriana ili walalie/ waatamie kwa pamoja.
Weka mayai 12 hadi 15 kwa kila kiota cha kuku 1 kulingana na umbo la kuku wako.
Kuku anaweza kutaga hadi mayai 30 kwa kila msimu wa kutaga unapofika. Unaweza kutumia mayai machache kati ya 30 kwa kumuatamishia kuku wako huku mayai mengine yakisubiri awamu ya pili ya kuatamiwa.Kwa mfano ukiwawekea kuku wako hao watano, Kuku 5 x Mayai 12 =Mayai 60.
Kwa kawaida kuku huatamia/hulalia mayai kwa siku 19 hadi 21/24 tu hadi anapototoa vifaranga. Hakikisha unawawekea kuku walioatamia chakula chenye viini lishe vya kutosha na maji mengi karibu na viota vyao ili wakitoka kwenye viota vyao wale chakula mara moja na kunywa maji kisha warudi haraka kwenye mayai yao. Hii itasaidia kuangua mayai yote 12/15 bila kuharibu yai hata moja.
Au hata yakiharikbika basi hayataharibika mengi kama ukiacha kuwawekea chakula waende kufukuzana na panzi na vyakula majalalani huko nje na kuchelewa kurudi kwenye mayai yao.
Wakati ukisubiria siku hizo 21/24 anza kujenga kibanda kidogo ndani ya banda kubwa ulilojenga awali au jikoni au andaa boksi kubwa na gumu kwaajili ya kutunzia vifaranga watakaoanguliwa ndani ya siku 21/24 zijazo.
Baada ya kuku hao 5 kuangua vifaranga wako 60 hapo ndipo kazi kubwa ya kulea vifaranga inapoanza. Elewa kuwa ili upate mafanikio haraka hakikisha kuwa kazi ya kulea vifaranga inakuwa yako na siyo ya kuku! Kwanza, Unatakiwa kuondoa na kuchoma moto/kufukia mabaki yote ya mayai na kuboresha usafi wa banda lote ili kuepusha magonjwa kama vile kuharisha, viroboto, papasi nk.
Hapo unaweza kuwatoa vifaranga wako wote 60 mmojammoja kadri wanavyoanguliwa hadi kufikia kifaranga wa mwisho, yaani Yule wa 60 na kuwaweka katika kibanda kidogo/boksi ulichokijenga na kuwawekea mayai mengine mama zao (yale 15/18 kati ya 30 uliyoyabakiza) ili waatamie tena kwa siku 21 hadi 24 zingine.
Unapotoa kifaranga kutoka kwa kuku aliyeatamia humfanya kuku Yule ashindwe kutoka kwenye mayai maana hana mtoto wa kulea.
Akimaliza kuangua mayai yote na ukamuwekea mengine ni rahisi kwake kuendelea kuatamia maana atasubiri kupata vifaranga na ndipo atajikuta amelalia kwa siku 21 zingine bila wasiwasi.
Kwa kufanya hivyo utakuwa tayari umejipatia vifaranga/kuku zaidi ya 100 ndani ya wiki 7 tu! Sasa Unatakiwa kuwajali sana kuku hawa wanaolalia kwa mara ya pili kwa kuwapa chakula cha kutosha, maji, majani ya makongwe, mchicha, mchunga nk ili wapate vitamini na madini mengine muhimu kwa afya zao.
Fanya hivyo hata watakapokuwa wametotoa na ukawanyang’anya vifaranga. Hii itawasaidia ili wasinyonyoke sana manyoya maana kuku wengi hunyonyoka manyoya wanapoatamia. Kwa kufanya hivi, kuku wako watakaa kwa wiki 2 hadi 3 bila vifaranga na kisha wataanza kutaga tena na kuatamia kama mwanzo.
NAMNA YA KULEA VIFARANGA.
Katika ulezi wa vifaranga kama kuku utawanyang’anya vifaranga vyao utatakiwa kuwajengea banda dogo (ndani ya banda kubwa/uzio) ili uwawekee chanzo cha joto kama taa/jiko la mkaa (kama ni sehemu/ majira ya baridi).
Kama utatumia jiko la mkaa unatakiwa kuacha kwanza hadi mkaa mweusi uwake wote ndipo uweke bandani maana mkaa ukitoa moshi unaweza kuathiri vifaranga vyako.
Angalia namna ya kuweka jiko lako la mkaa juu kidogo ili vifaranga wasiungue. Hakikisha taa yako haitoi moshi sana na haivujishi mafuta. Pia uwe na akiba ya mafuta ya taa ya kutosha.
Usiweke mafuta mengi kwenye taa maana inaweza kulipuka ikakuletea hasara. Vifaranga wasizidi 50 kwa boksi 1. Hakikisha umewasha taa/jiko lako ndani ya boksi saa tatu au zaidi kabla ya kuwaweka vifaranga ili chumba/boksi lipate joto kabla ya vifaranga kuwasili.
Njia hizi zinahitaji uangalifu wa hali ya juu sana kwani kuhatarisha/kuua vifaranga ni kuhatarisha maendeleo yako. Kama utaamua kutumia umeme pia ni vizuri zaidi maana inapunguza hatari zaidi.
Kwa hiyoa njia zote tatu unaweza kutumia jedwali lifuatalo ili kuweza kumeneji joto la kibanda cha vifaranga;
UMRI WA KUKU/VIFARANGA JOTO NDANI YA BOX/KIBANDA CHA KULELEA VIFARANGA JOTO NDANI YA CHUMBA/BANDA
Wiki 1 33-35oc 30-32oc
Wiki 2 30-33oc 27-29oc
Wiki 3 27-31c 24-26oc
Wiki 4 24-29oc 21-23oc
Wiki 5 26-27oc 22-23oc
Baada ya wiki ya 4/5 pasua box/watoe kwenye banda la kulelea ili walelewe kwa joto la kawaida la banda/chumba.
Kwa kawaida joto hupimwa kwa kipimajoto (thermometer), lakini kama huna kipimo hiki, njia rahisi ni kuwaangalia kulingana na tabia zifuatazo;
Kama vifaranga wamejikusanya sehemu moja basi joto ni kidogo bandani mwao, au kama wanaenda mbali na chanzo cha joto huku wanatanua mabawa yao na wakihema harakaharaka basi joto ni kali/ limezidi kiwango.
Pale watakapo tawanyika vizuri ndani ya boksi/kibanda cha kulelea huku wanakula na kunywa maji vizuri basi joto ni la wasta na ndilo linalofaa. Kama unatumia njia ya Boksi, basi unatikiwa kulipanua kulingana na ukuaji na mahitaji ya vifaranga vyako.
Vifaranga wako wape chakula cha vifaranga cha kutosha, maji safi na salama, majani mabichi ambayo hufungwa kwa kuning’inizwa kwa kamba,na CHANJO za minyoo nk ili wapate vitamin, madini na protini itakiwayo na kuzuia tabia ya kudonoana ili wakue vizuri.
Hakikisha kuwa chumba chao ni kisafi na hakina unyevunyevu wakati wote. Unyevunyevu husababisha ugonjwa wa baridi na hufanya vifaranga wajikunyate na kutetemeka na wanaweza kufa ghafla! Inashauriwa kuwa siyo salama kufuga aina nyingine ya ndege kama vile njiwa, bata, bata
mzinga nk kwa kuwachanganya na kuku maana kila aina ya ndege wanamagonjwa yao.
Hivyo kuwachanganya kutakufanya ushindwe namna ya kuwatibu wanapopatwa na ugonjwa.
Pia chawa wa njiwa huleta ugonjwa wa Ndui hasa kuku wanapoangua vifaranga wao.
Hapa ugonjwa unaweza kufyeka vifaranga wako wote 60/100 kama utafuata ushauri wangu!
Baada ya wiki 2 hadi 3 baada ya kuwanyang’anya vifaranga kuku wako wataanza tena kutaga mayai. Wakiatamia wote 5 Kama utaimarisha huduma kwao na kwa vifaranga/kuku wale 100 tayari utakuwa una kuku 105 au zaidi.
Kuku wale 5 wa mwanzo wakiatamia tena kwa siku 21 hadi 48 (kama utafuata mfumo ule wa mwanzo wa kuaatamishia mara 2) utajipatia vifaranga wengine 100 tena na hivyo kuwa na kuku zaidi ya 200 ndani ya miezi 5/6 tu!
Ukiwahudumia vifaranga wale wa mwanzo 100 vizuri kwa miezi 3 na nusu nao wataanza kutaga kama mama zao. kwahiyo, Chukulia walalie majike 5 wa mwanzo na majike 50 waliopatikana baada ya uzao wa kwanza kwa miezi ile 3 ya mwanzo utakuwa na mitetea 55.
Wote wakiatamia na watoe vifaranga 10 kila mmoja kwa siku zilezile 21 hadi 46, tayari utakuwa na vifaranga 550!
Sasa jumlisha na wale 150 waliobakia kati ya kuku 200 na wote wakakua vizuri utapata kuku na vifaranga zaidi ya 700! Jumlisha na 550 watakaototolewa na mama zao wale 5 wa kwanza na wale 50 wa uzao wa 1 na 2 kwa mara ya 2 si tayari utakuwa na kuku zaidi ya 1,200 ndani ya miezi 6 hadi 8 tu? Hivyo utajikuta unao kuku zaidi ya 1,000!
Kati ya kuku 1,000 ukisema utoe kuku 800 wa kuuza na ukiwauza kwa bei ya Tsh. 4,000 kwa kila kuku 1 tayari utakuwa na Jumla ya Tsh. 320,000/= ambazo unaweza kufanya mtaji wa mambo mengine au kuboresha mradi wako zaidi. Unafikiri hapo hujaanza kufikia lengo la kuku 1 akuletee shilingi Milioni 1?
Ukiendelea hivi inamaana kuku 1 atakuzalishia zaidi ya hapo.
BANDA LA KUKU.
Unatakiwa kuwa na banda bora la kufugia kuku ambalo litaweza kutunza kuku ili wasiweze kupatwa na madhara mbalimbali kama vile; kuliwa/kujeruhiwa na wanyama wakali, kuchukuliwa na wezi nk.
Lakini banda bora pia litawasaidia kuku kuhimili mabadiliko mbalimbali ya hali ya hewa yanayoweza kujitokeza.
Sehemu ambayo inafaa kwa ujenzi wa banda bora ni ile ambayo inaweza kufikika kwa urahisi, iwe na mwanga wa kutosha, isiwe na upepo mkali na isiyoruhusu maji kusimama au kuingia ndani.
Banda ni vema likawa la ukuta/mbao/ mabanzi.matete/mianzi imara ili lishikilie paa vizuri lisianguke. Kuta hizi zaweza kujengwa kwa matofali ya saruji/matope/kuchomwa/ mabanzi/mbao nk.
Katika kuezeka waweza kutumia mabati/vigae/nyasi. Banda ni vema likawa kubwa kulingana na kiasi cha kuku na umri walionao.
Kitu cha kuzingatia ni kwamba banda liwe na hewa ya kutosha. Kuku wanaofugwa ndani ni vema
wakatengenezewa uzio mpana (angalau Mita 8x10) ili wapate mahali wanapoweza kuota jua,
kupumzikia/kupunga hewa na kufanya mazoezi (wawekee kamba/bembea/ngazi ndani ya banda).
Hakikisha kuwa banda ni imara na hawatoki nje ya banda na kwenda mbali ili uweze kuwawekea chakula cha kutosha na maji na hata wale wanaotaga/kuatamia wapate chakula na kurudi haraka.
Banda likiwa kubwa na bora litapunguza magonjwa kwani litakuwa na hewa ya kutosh ambayo itasaidia kupunguza joto na unyevunyevu usio wa lazima bandani mwako. Hii itasaidia uingizaji oksijeni ya kutosha na kupunguza hewa chafu zenye madhara kwa kuku.
Pia litasaidia namna ya kufanya usafi kwa urahisi na kupunguza vumbi ambalo linaweza kusababisha kikohozi kwa kuku wako. Ni vema banda lisipungue Mita 3 kwenda juu. Mambo muhimu ndani ya Banda.
1. Sakafu nzuri (iliyotengenezwa kwa saruji/ udongo ili isituamishe maji. Isiwe na nyufa ili iweze kusafishwa kwa urahisi.
2. Hakikisha kuwa banda linakuwa na Viota (vitagio) vizuri kwaajili ya kutagia. Viota viwe na urefu wa Sentimita 30 na upana sentimita 30 na kina sentimita 35. Sehemuya mbele izibwe kwa sentimita 10 tu chini. Sehemu zote hizo zizibwe kwa ubao. Kama kuku wako ni wakubwa unaweza kuongeza upana, urefu na kina kiasi cha kutosha mfano, Upana na Urefu 35cm, kina 55cm nk.
Hakikisha kiota/kitagio kinakuwa na giza kiasi maana kuku hupenda kutaga mahala pa giza kidogo/palipojificha. Giza litasaidia kuku asiweze kula mayai au asiweze kudonoana na kuku wengine. Kiota pia kinatakiwa kiwe mahali ambapo ni rahisi kwa kuku kuingia na kutoka, pia iwe ni rahisi kusafisa.
Ndani ya kiota kuwekwe majani makavu/ maranda ya mbao laini na kinyunyize dawa ya unga ya kuzuia viroboto/utitiri kabla ya kuweka nyasi.
AIDHA, ni vizuri sana kuwawekea kuku wanaoatamia mayai wakati wa usiku maana ukimuwekea wakati wa mchana anaweza kuyaacha.
Kuku anayetarajiwa kuatamia ni vema akachunguzwa kama anao utitiri/viroboto/ chawa kwenye manyoya yake. Wadudu hawa humkosesha raha kuku anayeatamia na wengi huacha mayai na kukimbia/wasitulie kwenye viota vyao.
Hali inapelekea kuanguliwa kwa vifaranga wachache. Unaweza kumuona mtaalam wa mifugo kwa ushauri zaidi.
1. Banda liwe na vichanja maana kuku hupenda kulala juu ya vichanja maana nao ni ndege.
2. Vyombo safi na vizuri kwaajili ya chakula na maji.
3. Walazie majani makavu/maranda ya mbao/ makapi ya mazao sakafuni kwa banda zima.
HII NDIO SIRINYA MKOPO
Nichukue fursa hii adhimu, kwa kukupogeza sana wewe kwa kuendelea kusoma makala mbalimbali kupitia mtandao huu, kwani ni imani yangu kubwa sana, kama kweli yale ambayo unayojifunza kupitia mtandao huu na kuyaweka katika matendo basi maisha yako yatakuwa yamebadilika sana kwa kiwango kikubwa sana. Hivyo nikusihi ya kwamba uendelee kujifunza kwa kusoma kila mara kwa mara kupitia mtandao huu wa dira ya mafanikio, pia usisite kumshirikisha mwingine.
Basi nadhani nisizungumze sana niende moja kwa moja katika somo ambalo nmelikusudia, najua fika wapo baadhi ya watu kwao mikopo ni rafiki , wapo pia baadhi ya watu ambao mikopo kwao imekuwa ni adui mkubwa sana, hii ni kutokana na matokeo ya mikopo hiyo.
Pia mikopo hiyo ipo ya aina mbalimbali kwa mfano;
(a) mikopo midogo midogo- hii ni mikopo ambayo hutolewa kwa jamii, kwa ajili ya kuendeleza biashara ndogo ndogo. Lengo la mkopo huu husaidia kuongeza mtaji katika biashara ndogo ndogo ili kuwa biashara kubwa.
(b) Mikopo ya wafanyakazi- hii ni aina ya mikopo ambayo hulipwa wafanyakazi kwa ajili kuendesha maisha yao kiujumla. Na mara nyingi mishahara hili marejesho yake hukatwa kutoka mahali fulani kwenye mshahara wa mkopaji.
(c) Mikopo ya biashara- hii ni aina ya mikopo ambayo mara nyingi humsaidia mtu hasa katika suala la kuongeza mitaji katika biashara kubwa na kuifanya biashara hiyo kukua zaidi.
Hizo ni baadhi za aina ya mikopo ambayo hutolewa kwa wanajamii lakini zipo aina nyingi za mikopo. Lakini katika makala haya naomba nijikite zaidi katika siri ambazo zimejificha katika mikopo ya kibiashara maana huku ndiko ambako watu wengi hasa wafanyabiashara wengi waichukue mikopo hiyo, na watu wachache ndio ambao wana urafiki na mikopo hiyo ya kibiashara. Je nini kinachosababisha hali hiyo?
Zifuatazo ndiyo siri ya mkopo iliyojificha.
1. Usichukue mkopo kama biashara yako haifanyi vizuri.
Watu wengi hususani hawa wanaoichukia mikopo ya kibiashara, wengi wao huchukua mikopo hasa pale ambapo biashara inapokwenda vibaya, lakini kufanya hivi ni kosa kwa sababu wateja wengi huwa wamepotea hivyo ukichukua mkopo itakuwa ni kazi bure kwani wateja watakuwa wachache hivyo suala la marejesho kwako litakuwa ni suala gumu sana, ila ili kuufurahia mkopo wa kibiashara hakikisha unachukua mkopo wakati biashara inakwenda vizuri, kwani kufanya hivi wateja watakuwa wengi pia itakuwa ni rahisi kwako kurejesha marejesho ya mkopo huo.
2. Chukua mkopo kwa lengo ulilokusudia.
Mara zote watu wengi huuchukia mkopo wa kibiashara kwa sababu malengo ya kuchukua mkopo huo hufanya kazi ambazo huzikustaili, kwa mfano utakuta mtu amechukua mkopo kwa kuendeshea biashara lakini cha ajabu pale mtu huyo apewapo mkopo huo utashangaa anafanyia kitu kingine kama vile ulipaji karo, kodi ya nyumba n.k. lakini kufanya hivi ukumbuke ya kwamba ni kupoteza maono sahihi ya kibiashara na mwisho wa siku kupelekea biashara kufa.
Ni vyema ukayazingatia hayo kabla ya kuamua kuchukua mkopo wowote ule. Kufanya hivo kutakusaidia sana kukuza biashara yako.
Jisajili kwenye:
Maoni (Atom)


















